
Maalim Seif Shariff Hamad, Mgombea wa Urais wa Zanzibar katika
uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka jana kupitia Chama cha Wananchi (CUF),
amesema CUF haitashiriki uchaguzi wowote chini ya Tume ya Jecha Salim
Jecha, anaandika Josephat Isango.
Akizungumza na MwanaHALISI Online Hoteli ya Serena ambapo yupo kwa
mapumziko baada ya kulazwa, Maalim Seif amesema kuwa kama yatatokea
maridhiano yatakaoongozwa na kusimamiwa na taasisi huru za kidemokrasia,
...