Vita vimezuka kati ya waislamu na wahindi katika mji wa Gujarat huko
India baada ya picha kuwekwa katika mtandao wa kijamii unaokosea dini ya
Kiislamu kughadhabisha wakaazi wa eneo hilo.
Wakaazi wa dini hizo mbili wamerushiana mawe na kuchoma magari na
kusasabisha wengi kujeruhiwa huku mmoja akidungwa kisu katika vurugu
hilo.
Afisa mkuu katika eneo hilo amesema kuwa huduma za mtandao zote zikiwemo
za simu zimesimamishwa hadi kesho ili kupunguza uenezi wa hasira kwa
wananchi.
Kamishna wa polisi katika eneo hilo D.J Patel amesema mwanamume
aliyeweka picha hiyo kwa mtandao wa kijamii ametiwa mbaroni pamoja na
watu 200 wanaoshukiwa kuanzisha vita hivyo
Oct 1, 2014
Mtandao wa kijamii wazua vita vya kidini nchini India
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment