Mar 28, 2016

Israel imeua watoto 50 Wapalestina tokea Oktoba


Israel imeua watoto 50 Wapalestina tokea Oktoba
Wanajeshi wa Utawala haramu wa Israel wameua watoto 50 Wapalestina tokea Oktoba mwaka jana, wakati ilipoanza Intifadha au mwamko mpya wa Palestina. 
 
Kwa mujibu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kutetea Watoto- Tawi la Palestina, ukosefu wa uchunguzi huru na wa wazi kuhusu ukatili huo wa Israel ni jambo ambalo limepelekea kuendelea kuuawa watoto Wapalestina kiholela. 

Ayed Abu Qtais, wa jumuiya hiyo amelalamika kuwa Umoja wa Mataifa umefeli kutekeleza majukumu yake kuhusu kutetea haki za watoto Wapalestina. 

Tangu mwanzoni mwa mwezi Oktoba mwaka uliopita wa 2015 hadi sasa maeneo mbalimbali ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu yamekuwa yakishuhudia wimbi la malalamiko ya upinzani dhidi ya siasa za kichokozi za utawala wa Kizayuni na njama za utawala huo za kupotosha utambulisho wa Baitul Muqaddas pamoja na mpango wake wa kuugawa kiwakati na kimahali msikiti mtukufu wa Al-Aqsa. Wimbi hilo la malalamiko limekuwa maarufu kwa jina la Intifadha ya Quds. 

Wapalestina zaidi 200 wameshauawa shahidi tangu ilipoanza Intifadha ya Quds mwezi Oktoba mwaka jana hadi hivi sasa.

0 comments:

Post a Comment