Mar 28, 2016

'Kampeni za urais zinaiaibisha Marekani'


'Kampeni za urais zinaiaibisha Marekani'
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry amekiri kuwepo utovu wa nidhamu katika kampeni za uchaguzi wa rais nchini humo na kusema jambo hilo limepelekea Marekani kuaibika kimataifa.

Katika mahojiano na kanali ya televisheni ya CBS, Kerry amesema, "kila mahala ninapoenda, kila kiongozi ninayekutana naye, wananiuliza ni nini kinachoanedelea Marekani. Hawawezi kuamini yanayojiri na naweza kusema wameshangazwa."

Kauli hiyo ya Kerry inaonekana kuelekezewa wagombea wawili wanaowania uteuzi wa chama cha Republican kugombea urais, Donald Trump na Ted Cruz ambao wamekuwa wakitoa matamshi makali dhidi ya Uislamu na jamii ya watu weusi nchini Marekani. 

Trump na Cruz wametaka kuchukuliwe hatua kali za kuwadhibiti Waislamu na kuzuia wahamiaji wasiokuwa wazungu kuingia nchini humo. Halikadhalika wagombea hao wawili wenye misimamo ya kufurutu wada wamekuwa wakitusiana hadharani kuhusu masuala mbali mbali wakiwemo wake zao.

Hivi karibuni pia Trump, alitishia kuwa, iwapo hatateuliwa na chama hicho, basi watu wasubiri ghasia na machafuko kote Marekani.

Kerry ameongeza kuwa matamshi ya wagombea hao wawili yamepelekea itibari ya Marekani kutoweka duniani.

0 comments:

Post a Comment