Maelezo: Munira









































MUNIRA MADRASA & ISLAMIC PROPAGATION ASSOCIATION







ACCOUNTING FOR FINANCIAL AFFAIRS




AS AT :  30-06-2013

STRUCTURE









S/NO: NATURE OF ASSETS / LIABILITY QUANTITY U/PRICE VALUE

FIXED ASSETS
1 BUILDING 1 21,000,000.00

2 FURNITURE 26 635,000.00

3 FITTINGS 690,000.00

RADIO  1 140,000.00

3 MACHINES & EQUIPMENTS 5,605,000.00

4 LAND 1 10,000,000.00

38,070,000.00

CURRENT ASSETS

1 CASH 365,000.00

2 STOCK  Books 400 1,500.00 600,000.00

3 DEBTORS

4 PRE-PAYMENTS
965,000.00



LIABILITIES
1 CREDITORS 492,000.00

2 LOANS

3 DUE PAYMENTS


WORKING CAPITAL 473,000.00




NET EQUITY 38,543,000.00


NOTE

DIFFERED PAYMENTS
ARCHITECTURAL DRAWINGS-MLANDIZI SITE- FOR SCHOOL 3,500,000.00
ARCHITECTURAL DRAWINGS--MAGOMENI- FOR MADRASA 2,000,000.00

BANK A/C NO:00112-00592-20001 AMANA BANK





































MUNIRA MADRASA &ISLAMIC PROPAGATION ASSOCIATION







CAPACITY BUILDING 2013/2014









OFFICE MACHINES AND ACCESSORIES









1 PHOTOCOPIER MACHINE 1 6,000,000.00 6,000,000.00

2 UPS (STABILIZER) 1 600,000.00 600,000.00

3 SERVICE CHARGES  400,000.00 400,000.00

4 PRINTER MULTIPURPOSE 1 980,000.00 980,000.00

5 LAMINATION MACHINE 1 70,000.00 70,000.00

6 BINDING MACHINE  1 75,000.00 75,000.00

7 STAPPLER MACHINE ( H / D ) 1 45,000.00 45,000.00

8 PUNCH MACHINE  ( H / D ) 1 25,000.00 25,000.00

9 PAPER CUTTER  1 35,000.00 35,000.00

10 DESK TOP  COMPUTERS  2 350,000.00 700,000.00

11 LAP TOP COMPUTER 1 850,000.00 850,000.00

12 DIGITAL CAMERA 1 1,200,000.00 1,200,000.00






TOTAL 10,980,000.00










































   MUNIRA MADRASA &ISLAMIC PROPAGATION ASSOCIATION






CAPACITY BUILDING COSTS MONTHLY SIX MONTHS ANNUALLY

ADMINISTRATIVE PERSONNEL

1 EXECUTIVE SECRETARY 1 300,000.00 1,800,000.00 3,600,000.00
2 ADMINISTRATIVE SECRETARY 1 200,000.00 1,200,000.00 2,400,000.00
MADRASA TEACHERS 6 900,000.00 5,400,000.00 10,800,000.00
3 OFFICE SECRETARY 1 150,000.00 900,000.00 1,800,000.00
4 OFFICE ASSISTANT 1 100,000.00 600,000.00 1,200,000.00
WATCHMAN 1 180,000.00 1,080,000.00 2,160,000.00
CAR PARKS REGISTRER 1 150,000.00 900,000.00 1,800,000.00
TOTAL 1,980,000.00 11,880,000.00 23,760,000.00
**********************************************************************************
**********************************************************************************



MUNIIRA MADRSA AND ISLAMIC PROPAGATION ASSOCIATION
PROFILE 
1990-2013

JINA LA TAASISI;       MUNIIRA MADRASA AND ISLAMIC PROPAGATION
                                    ASSOCIATION.



ANUANI;                      90536,DAR ES SALAAM,



SIMU YA MEZANI;       255 222172624



SIMU YA MKONONI;    0713 44 16 39/ 0719 46 47 00/ 0713 43 43 37.



BARUA PEPE;             muniiramadrasa@yahoo.com



MTANDAO;                  www.muniramadrasa.blogspot.com


ACCOUNT;                    001120059220001,AMANA BANK,TANDAMTI BRANCH.
                                025147013004 – Kenya Commercial Bank, Uhuru Branch,


MAKAZI;                      MAGOMENI MAKUTI,



MTAA;                         KIDUGALO,MAKUTI ‘B’



MANISPAA;                 KINONDONI,



MKOA;                         DAR ES SALAAM.

TAIFA;                         TANZANIA.



Muniira Madrasa And Islamic Propagation Association ni taasisi ya kidini iliyoanzishwa mwaka 1990 na kupata usajili (No S.A 16751) mwaka 2009 kupitia ofisi ya msajili wizara ya mambo ya ndani.

Taasisi hii imeanzishwa kwa sura ya madrasa (ikijulikana kwa jina la Madrasat Muniiral Islamiyyah) ikiwa na wanafunzi 18 na walimu watatu.

Idadi ya wanafunzi iliendelea kupanda siku hadi siku kutokana na wazazi na walezi kuridhishwa na elimu bora,malezi na maadili mema yanayotolewa na madrasa hii.

Taasisi hii imeanzishwa kwa malengo makuu matatu ambayo ni;-
            01- Kutoa elimu ya kiislamu kwa rika zote.      
            Katika lengo hili Taasisi hii inatoa elimu kwa njia mbali mbali ikwemo;-
                                                               i.      Kutoa elimu kwa njia ya darasani (ana kwa ana)
                                                             ii.      Kutoa elimu kwa njia ya vipeperushi,
                                                            iii.      Kutoa elimu kwa njia ya tenzi na mashairi,
                                                           iv.      Kutoa elimu kwa njia ya maigizo ya jukwaani,
                                                             v.      Kutoa elimu kwa njia ya semina,
                                                           vi.      Kutoa elimu kwa njia ya mihadhara,
                                                          vii.      Kutoa elimu kwa njia ya ujumbe mfupi (sms)
                                                        viii.      Kutoa elimu kwa njia ya mtandao (e mail),
                                                           ix.      Kutoa elimu kwa njia ya kutunga vitabu
                                                             x.      Kutoa elimu kwa njia ya ukurasa wa tovuti (blog).




Aidha sasa kwa sasa Taasisi hii ina endesha Darsa zifuatazo;-
                                    Darsa la watoto wadogo (wenye umri wa miaka mitatu hadi kumi
                                    Na nane).
                                    Darsa za wenye umri wa miaka kumi na nane hadi miaka 29.
                                    Darsa la akina mama kwa umri mchanganyiko.
                                    Darsa la chekechekea (elimu ya awali).

            02- Kuisaidia jamii inayotuzunguka kwa kadri ya uwezo wetu,
Taasisi hii inajishughulisha na kuwasidia wana jamii wanaotunguka kwa kuwapatia sehemu ya mahitaji kwa kadri tunavyomudu.

Fikra hii tumeipata baada ya kufanya fafiti fupi iliyotupa ufahamu ya kugundua mahitaji waliyo nayo baadhi ya akina mama hasa wajane na wazee,lakini pia mahitaji yanayowalazimu watoto yatima na watoto wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi.

Katika kuliendea hilo tulichukua hatua ya kuwaorodhesha na hatimaye kuwafariji kwa hali na mali kadri ya pale tunapo pata nafasi ya kufanya hivyo.

Kwa mujibu wa kumbukumbu za hivi karibuni ni kwamba katika kipindi cha mwaka 2012 na 2013 jumla ya waliosaidiwa na Taasisi hii ni kama ifuatavyo;-
1.       Wajane 50 walipewa mitaji ya biashara (siyo mikopo) kwa viwango tofauti kati ya shilingi elfu thelathini na shilingi laki moja kwa kila mmoja.
2.       Wajane wanane vyarahani vinane.
3.       Wajane wanne majokofu (frij) manne.
4.       Wazee arobaini vyakula (mchele,sukari,sembe na maharagwe).
5.       Yatima 50,walipewa vyandarua.
6.       Yatima 50 walipewa sare za shule
7.       Yatima 110 walilipiwa ada za masomo (viwango tofauti) katika shule za sekondari.
8.       Watoto 50 walipatiwa matibabu kwa gharama matibabu kati ya shilingi elfu kumi na tano hadi elfu khamsini.
9.       Kuwatembelea na kuwafariji wagonjwa mahospitalini (katika siku kuu ya iddil hajj kwa kila mwaka)
(Tunatoa misaada hiyo baada ya kuwaomba wapenda kheri na sisi viongozi kujitolea binafsi)

            03- Kusaidiana na serikali katika kufikisha maagizo mema.
Tumekuwa tunawajibika kusaidiana na serikali katika kufikisha maagizo mema kwa jamii,kama kupiga vita madawa ya kulevya,mmomonyoko wa maadili,kupinga dhulma,kukemea wizi,ufisadikutoa elimu ya afya nk,

Tumekua tunayafanya haya kwa kukabiliana na mtu mmoja mmoja au kwa vikundi kwa kutumia njia mbalimbali ikiwemo ya mihadhara na darsa za ndani.

MAHUSIANO;
Tuna mahusiano mazuri kati ya taasisi hii na serikali,aidha tuna mahusiano mazuri baina yetu na Taasisi nyengine zisizo za kiserikali.

MAWASILIANO;
Kwa kufahamu ya kwamba mawasiliano ni muhimili muhimu katika kufanikisha malengo yetu,mbali ya mambo mengine tumeweka utaratibu wa kutumia mawasiliano kwa njia zifuatazo;-
  1. Mawasiliano kwa njia ya barua (sanduku la posta 90536,Dar es salaam)
  2. Mawasiliano kwa njia ya simu za mkononi
  3. Mawasiliano kwa njia simu ya mezani
  4. Mawasiliano kwa njia ya emal
  5. Mawasiliano kwa njia ya blog
Na mawasiliano ya ana kwa ana .(tunataraji kuwa na web site ikifika mwaka 2014 inshaa ALLAH)

 MALENGO;
Tuna malengo ya muda mrefu na malengo ya muda mfupi.
Malengo ya muda mrefu ni pamoja na
1.       Kuwa na shule yenye hadhi ambayo itakuwa inafundisha kwa wakati mmoja elimu ya dini na elimu ya mazingira (intergred) kwa ngazi ya awali hadi elimu ya kati,yenye jengo la utawala,maabara,zahanati,karakana,madrasa,msikiti na nyumba za maimamu,walimu wa madrasa na walimu wakuu wa shule.
Mwenyeezi mungu akipenda mradi huu (kwa tathmini ya mwaka 2011,utagharimu Tsh Bilioni tatu nukta tatu),utakuwa maeneo ya mlandizi wilaya ya kibaha mkoa wa pwani (tunayo ardhi yenye ukubwa wa heka kumi,taraibu za upimaji na upatikanaji wa hati umeshaanza).
2.       Kuanzisha mradi wa kilimo na ufugaji maeneo ya mkuranga,(tulianza mwaka huu kwa majaribio kilimo cha mihogo,lakini mafanikio hayakuwa mazuri).
3.       Kumiliki madrasa ya kisasa (eneo la magomeni makuti) yenye vyumba vya madarasa manne,ofisi mbili,library moja,ukumbi wa mikutano,stoo,vyoo sita na bafu tatu,(kwa sasa tupo pembezoni mwa nyumba ya msamaria mwema).

MAFANIKIO;
Tangu Taasisi hii ianzishwe mwaka 1990 hadi kufikia mwaka 2013,kuna mafanikio mengi yamepatikana,ikiwemo;-
  1. Kuwaunganisha wazazi wa kiislamu wa maeneo haya na kuwa familia moja.
  2. Kuwaunganisha watoto wa kiislamu wa maeneo haya na kuwa familia moja.
  3. Kuwaunganisha wazazi na watoto wa kiislamu wa maeneo haya na watoto na
      Wazazi wa kiislamu wa maeneo mengine.
  1. Kuwafanya watoto na hata wazazi wa kiislamu kuwa na elimu tofauti na hali
      Waliyokuwa nayo kielimu na kimaadili kabla ya kuanzishwa kwa taasisi hii.
  1. Kuwa na mahusiano mema ya kielimu,kimawasiliano na hata ya kiutendaji na
      Na baadhi ya Taasisi mbali mbali na mtu mmoja mmoja.
  1. Kuwa na mahusiano mema na serikali.
  2. Wajane,wazee,wagonjwa,yatima na watoto wanaoishi katika mazingira magumu kufaidika na misaada inayotolewa na taasisi.

MENGINEYO;
Taasisi hii imetenga kila jumamosi ya kwanza katika kumi la mwisho wa mwezi wa Ramadhan,kufuturu pamoja kama familia moja.
Tukio hili lina wahusiha waalimu,wazazi,walezi,wanafunzi,wajane,wazee,yatima,watoto wanaoishi katika mazingira magumu na waislam ambapo takriban watu mia nne tunafuturu nao pamoja.
usiku wa kuamkia iddil fit huwa tuna kesha kwa kupita katika majumba ya watu ambao hali zao ni duni (tumewaorodhesha) na kuwagawia zakaatul fitri kwa lengo la kuwataka wasinyongeke na wafurahie iddil fitri wao na familia zao.
Ili kufanikisha zoezi hilo,huwa tunakusanya zakatul fitri kutoka kwa wazazi na watu wengine.


CHANGAMOTO;
Tunakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo;-
  1. Taasisi kutokua na miradi,vyanzo vya mapato.
  2. Taasisi kutokuwa na uwezo wa kuwalipa waalimu na watendaji wengine (kwani wanajitolea tu).
  3. Taasisi kutokuwa na jengo (madrasa) la kudumu (hofu yetu inawezekana waliotuhifadhi watakapobadilika kiimani au kimaslahi ikawa ndiyo sababu ya kupotea na kusambaratika kwa mafanikio yote yaliyopatikana katika taasisi hii tokea mwaka 1990 na kuyeyusha ndoto njema kadhaa za taasisi hii,hili linatuathiri sana kifikra).

WITO;
Tunaiomba serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania,Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,mabalozi mbalimbali,Taasisi za kiraia,mashirika ya kidini na yasiyo ya kidini ndani na nje ya nchi,watu binafsi na hata mataifa mbalimbali,kuiunga mkono taasisi hii ili kufikia malengo yaliyojiwekea ambapo tuna amini malengo haya yakifikiwa itakuwa ni faida kwa jamii mzima ya Watanzania na Afrika Mashariki.