Feb 4, 2015

Wabunge watwangana makonde


 http://salaamfm.com/wp-content/uploads/2015/02/isiooooo.jpg
Wabunge wa kaunti ya Isiolo, wamelishana makonde mbele  ya umma, baada ya kutofautiana vikali kuhusu tarehe rasmi ya ufunguzi wa vikao vya bunge la kaunti hiyo mwaka huu.


Duru za kuaminika zinaarifu kuwa kumekuwa na tofauti kali kati ya gavana godana Doyo, na spika wa bunge hilo Mohamed Tubi kuhusu tarehe ya ufunguzi rasmi ya Bunge hilo mwaka huu.


Tubi ambaye ni spika wa bunge hilo amesema kuwa bunge hilo linafaa kufunguliwa wiki ya pili ya mwezi februari huku gavana akitaka bunge hilolifunguliwe hii leo jambo ambalo baadhi ya wabunge wamepinga vikali.


Makundi hayo mawili yamekuwa yakitofautiana vikali kuhusu uongozi wa kaunti hiyo,huku wabunge wanaounga mkono spika wakidai kuwa gavana anania ya kukandamiza majukumu ya wabunge hao.

0 comments:

Post a Comment