
Wabunge wa kaunti ya Isiolo, wamelishana makonde mbele  ya umma, 
baada ya kutofautiana vikali kuhusu tarehe rasmi ya ufunguzi wa vikao 
vya bunge la kaunti hiyo mwaka huu.
Duru za kuaminika zinaarifu kuwa kumekuwa 
na tofauti kali kati ya gavana godana Doyo, na spika wa bunge hilo 
Mohamed Tubi kuhusu tarehe ya ufunguzi rasmi ya Bunge hilo mwaka huu.
Tubi ambaye ni spika wa bunge hilo amesema 
kuwa bunge hilo linafaa kufunguliwa wiki ya pili ya mwezi februari huku 
gavana akitaka bunge hilolifunguliwe hii leo jambo ambalo baadhi ya 
wabunge wamepinga vikali.
Makundi hayo mawili yamekuwa yakitofautiana
 vikali kuhusu uongozi wa kaunti hiyo,huku wabunge wanaounga mkono spika
 wakidai kuwa gavana anania ya kukandamiza majukumu ya wabunge hao.
Feb 4, 2015
Wabunge watwangana makonde
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


 
 
 
 
 





0 comments:
Post a Comment