
Malalamiko na maswali kuhusu mirathi na talaka jana yalitawala 
katika Maonyesho ya Wiki ya Sheria, yaliyohitimishwa katika Viwanja vya 
Mnazi Mmoja. 
Akizungumza katika maonyesho hayo, Jaji Kiongozi, Shaaban Lila alisema Watanzania wengi hawana uelewa wa masuala ya kisheria.
                
              
Jaji Lila alisema lengo la maonyesho hayo lilikuwa ni kuwafafanulia wananchi kuhusu huduma na taratibu za utendaji wa Mahakama.
                
              
Msimamizi wa Kitengo cha Masuala ya Mirathi katika
 maonyesho hayo, Janeth Mwanisau alisema wanawake wengi walijitokeza 
hususan wajane. Alisema kutokana na unyeti wa tatizo la mirathi, ndiyo 
maana limetenganishwa na masuala mengine.
                
              
“Wanawake wamefika na kuuliza maswali huku 
wakieleza malalamiko yao ya kutengwa au kutokushirikishwa katika 
kufungua mirathi,” alisema Mwanisau.
                
              
Jaji Mkuu, Mohamed Chande alisema kaulimbiu ya 
maadhimisho hayo ilikuwa ni ‘Fursa ya kupata haki ni wajibu wa Serikali,
 Mahakama na wadau wote,’ na ililenga kuongeza uelewa wa wananchi. 
“Tulichagua kaulimbiu hii kwa sababu tunataka huduma zetu ziwafikie kwa 
haraka.
Nimeambiwa wananchi wameuliza maswali mengi ambayo wanasheria tunayaona ya kawaida lakini kwao ni magumu ,” alisema Jaji Chande.
Nimeambiwa wananchi wameuliza maswali mengi ambayo wanasheria tunayaona ya kawaida lakini kwao ni magumu ,” alisema Jaji Chande.


 
 
 
 
 





0 comments:
Post a Comment