Oct 9, 2013

MORRIS KUSHTAKIWA NOVEMBER


 MUHAMMAD MURSI

Aliyekuwa Rais wa Misri Mohammed Morsi aliyeng'olewa mamlakani atafunguliwa mashtaka mwezi Novemba tarehe nne.
Bw Morsi atashatakiwa kwa kosa la uchochezi na mauaji pamoja na wanachama kumi na wanne wa kundi Muslim Brotherhood.
Mashtaka hayo yanahusiana na mauaji ya waandamanaji saba wakati wa vurugu kati ya wafuasi wa upinzani na wafuasi wa Muslim Brotherhood nje ya ikulu ya rais mjini Cairo mwaka uliopita.

Kupinduliwa kwa bwana Morsi kumesababisha maandamano ya kupinga na kumuunga mkono kutoka kwa wafuasi na wapinzani na wafuasi wake na baadhi wameuawa na vikosi vya kijeshi.

Morsi atashtakiwa na viongozi wengine kumi na wanne wa vuguvugu la Brotherhood.

Amekuwa akizuiliwa katika eneo lisilojulikana tangu alipoondolewa mamlakani tarehe 3 mwezi Julai.

Mamia ya watu wanataka arejeshwe mamlakani na wengi wao wakiwa wafuasi wa vuguvugu la Brotherhood. Wengi wa wafuasi hao wameuawa kwenye makabiliano na vikosi vya usalama tangu Morsi alipong'olewa madarakani.

Zaidi ya watu hamsini walifariki kutokana na ghasia hizo siku ya Jumapili.

Mahakama ya rufaa mjini Cairo iliamua kuwa Morsi na wenzake 14 akiwemo Mohammed al-Beltagi na Essam al-Erian, wanaweza kufunguliwa mashtaka katika mahakama ya uhalifu.

Wendesha mashtaka walitangaza kuwa mwezi jana walifunguliwa mashtaka ya uchochezi kuhusiana na ghasia nje ya ikulu ya Rais mjini Cairo.

0 comments:

Post a Comment