Sep 25, 2013

Serikali ya Misri yaisakama Muslim Brother Hood


Hili ni  Jengo lililoshambuliwa la chama cha udugu wa Kiislamu mjini Cairo.

Serikali ya Misri imeyafunga makao makuu ya gazeti "Uhuru na Haki" ambalo linalomilikiwa na chama cha Udugu wa Kiislamu ikiwa ni hatua ya mwanzo yenye lengo la kuvurga kabisa harakati za chama hicho. 

Katika taarifa yake iliyotolewa leo (25.09.2013) katika mtandoa wa facebook, chama cha Udugu wa Kiislamu kimesema "Sisi waandishi habari wa gazeti la Uhuru na Haki tunalaani kitendo cha vikosi vya usalama kufunga makao makuu ya gazeti".
Usiku wa kuamkia leo, jeshi la polisi lilizishambulia ofisi hizo na kuondoa nyaraka kadhaa zilizokuwemo. 

Chanzo kimoja kutoka katika kitengo cha usalama cha Misri kimesema hatua hiyo inatokana na uamuzi wa mahakama wa Jumatatu, wa kupiga marufuku chama hicho na kuamuru kudhibitiwa hazina yake.

Mfuasi wa chama cha Udugu wa Kiislamu
Akiendeleza kutoa ufafanuzi kuhusu namna wanavyoendesha operesheni hiyo chanzo hicho kimesema uamuzi wa mahakama ambao umesababasha kutekelezwa kwa hatua hiyo kunatokana na kuwepo kwa mashitaka ya kuchochea vurugu pamoja na vitendo vya ugaidi kulikoteka katika siku za hivi karibuni.

Mwezi Julai mwaka huu, jeshi lilimuondoa madarakani rais Mohamed Mursi ambapo pia chama chama chake cha Udugu wa Kiislamu kimeshuhudia mikasa ya mamia ya wanachama wake kuuwawa na wengine maelfu kukamatwa tangu wakati huo.

0 comments:

Post a Comment