Mar 5, 2015

Shule za New York kufungwa Sikukuu za Idi mbili


Meya wa jiji la New York nchini Marekani, Bill De Blasio, ametangaza kuwa shule zote za umma katika mji huo zitakuwa zikifungwa kila mwaka wakati wa Sikukuu mbili muhimu za Kiislamu za Idul-Fitr na Idul-Adh’ha.
Hatua hiyo inalenga kuonyesha heshima kwa Sikukuu hizo mbili za Waislamu. 

Meya De Blasio amesema uongozi wa jiji la New York umeona pana haja ya kuweko na usawa katika kutambua na kuheshimu shughuli muhimu za watu wa dini mbalimbali mjini humo. 

New York ina wanafunzi wasiopungua milioni 1.1 katika shule za umma. 

Majimbo kadhaa ya Marekani yakiwemo ya Massachusetts, Michigan and New Jersey katika miaka ya hivi karibuni yameorodhesha sherehe za Idul-Fitr na Idul-Adh’ha kwenye kalenda ya matukio kwenye shule zao.

Baadhi ya wachambuzi wanasema hatua hiyo ni aina fulani ya mkakati wa  kuwapumbaza Waislamu wa Marekani ambao kwa hivi sasa wanakabiliwa na mashinikizo kutoka kwa vyombo vya usalama na vya kijasusi vya nchi hiyo kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi.

0 comments:

Post a Comment