
 Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Profesa John Nkoma.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewataka viongozi wa 
dini kutumia nafasi kukemea juu ya matumizi mabaya ya mitandao ya 
kijamii kwa waumini wao na kuelimisha madhara yanayoweza kusababishwa na
 teknolojia hiyo katika jamii.
                
              
Hatua hiyo ya TCRA imekuja kufuatia kukithiri kwa 
vitendo vinavyoashiria kutumika vibaya kwa mitandao ya kijamii kama njia
 ya mawasiliano hali inayochangia kuzidi kuporomoka kwa maadili.
                
              
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Profesa John Nkoma alisema
 lengo la kukutana na viongozi hao ni kuwapa elimu kuhusiana na madhara 
ambayo jamii inaweza kupata kufuatia ongezeko la matumizi mabaya ya 
mitandao.
                
              
“Mitandao ni mizuri sana lakini tatizo ni jinsi 
inavyotumika watu wamekuwa wakifanya mambo ya ajabu tena bila kuwa na 
hofu ya Mungu ndiyo maana tumerudi kwenu viongozi wa dini mtusaidie 
katika hili:
                
              
Kwa kutumia nafasi zenu tuna imani mtawaelimisha 
waumini ili waelewe kuwa kusambaza ujumbe unaoashiria uchochezi ni kosa 
kisheria na inaweza kuwa dhambi kwani hakuna ambaye angependa amani 
ivunjike”


 
 
 
 
 





0 comments:
Post a Comment