Feb 4, 2015

Viongozi wa Dini watakiwa kuinadi mitandao ya kijamii

 
 Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Profesa John Nkoma.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewataka viongozi wa dini kutumia nafasi kukemea juu ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii kwa waumini wao na kuelimisha madhara yanayoweza kusababishwa na teknolojia hiyo katika jamii.

Hatua hiyo ya TCRA imekuja kufuatia kukithiri kwa vitendo vinavyoashiria kutumika vibaya kwa mitandao ya kijamii kama njia ya mawasiliano hali inayochangia kuzidi kuporomoka kwa maadili.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Profesa John Nkoma alisema lengo la kukutana na viongozi hao ni kuwapa elimu kuhusiana na madhara ambayo jamii inaweza kupata kufuatia ongezeko la matumizi mabaya ya mitandao.
“Mitandao ni mizuri sana lakini tatizo ni jinsi inavyotumika watu wamekuwa wakifanya mambo ya ajabu tena bila kuwa na hofu ya Mungu ndiyo maana tumerudi kwenu viongozi wa dini mtusaidie katika hili:
Kwa kutumia nafasi zenu tuna imani mtawaelimisha waumini ili waelewe kuwa kusambaza ujumbe unaoashiria uchochezi ni kosa kisheria na inaweza kuwa dhambi kwani hakuna ambaye angependa amani ivunjike”

0 comments:

Post a Comment