OIC katika moja ya mikutano yake
Mawaziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa
nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC wamesisitiza
udharura wa kukabiliana na njama za kutaka Uislamu uogopwe.
Wakizungumza
kwenye mkutano wa kila mwaka pambizoni mwa kikao cha Baraza Kuu la
Umoja wa Mataifa, Mawaziri wa Mambo ya Nchi za Nje wanachama wa OIC
wameitaka jamii ya kimataifa kukomesha vitendo vya kichochezi na
uchokozi dhidi ya Waislamu.
Taarifa inasema kuwa, juhudi zaidi zinapasa
kufanyika kwa lengo la kuimarisha vigezo vya kuishi pamoja sambamba
licha ya kuwepo utamaduni unaotofautiana.
Wanachama wa Jumuiya ya
Ushirikiano wa Kiislamu OIC wamesisitiza kwamba, umma wa Kiislamu
unapasa kuipatia kipaumbele kadhia ya Palestina na Quds Tukufu na
kuzitaka nchi zote wanachama kuiunga mkono serikali na wananchi wa
Palestina ili waweze kufikia malengo yao likiwemo suala la kuundwa nchi
huru na mji mkuu wake ukiwa Quds Tukufu.
Mawaziri wa Mambo ya Nchi za
Nje wanachama wa OIC wamelaani kiburi cha utawala wa Kizayuni wa Israel
cha kuendeleza ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika
maeneo ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na Quds.
Taarifa ya OIC
imeeleza kuwa, ugaidi ni hatari na wala haufungamani na nchi, dini wala
utaifa na kusisitiza kwamba nchi za Kiislamu na Waislamu wamekuwa
wahanga wakubwa wa ugaidi.
0 comments:
Post a Comment