Jan 7, 2015

Viongozi wa Dini wawaanika Panya Road

Baadhiya viongozi wa dini hapa nchini wamezungumzia vurugu zilizofanywa wiki iliyopita sehemu kadhaa ya jijii Dar es Salaam na vijana wanaosadikika kuunda kundi linalojulikana kama Panya Road.

 Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa, amesema kuwa ukosefu wa ajira ni moja ya sababu zinazozalisha makundi ya ajabu, hivyo serikali inapaswa kujipanga na kutengeneza mifumo ya ajira kwa vijana ili kuwaepusha kujiingiza katika makundi tishio na hatari. 

Ameongeza kuwa, vijana hao wanavamia, kupora na kuumiza watu hovyo  hovyo na kwamba ukosefu wa ajira kwa vijana ni bomu kubwa na baya sana zaidi hata ya al Shabbab.

Naye Mchungaji Ifrahimu Mwansasu wa Kanisa la Hosana Life Mission, amesema kwamba makundi hayo ya uhalifu yanasababishwa na malezi mabaya ya kiimani na kitabia, kitu alichokiri kwamba hata yeye amewahi kupitia akiwa kijana kabla ya kuokoka na kuitaka serikali ikae nao na kujua sababu ya vijana hao kuwa hivyo.
 
Mwishoni mwa wiki iliyopita, kundi la Panya Road lilizua tafrani kubwa jijini Dar es Salaam baada ya kuwavamia, kuwapora na kuwajeruhi watu katika maeneo mbalimbali ya mji huo, lakini Jeshi la Polisi chini ya Kamanda Suleiman Kova lilifanikiwa kudhibiti kundi hilo.

0 comments:

Post a Comment