Nov 15, 2014

Mahakama Uswisi yaondoa marufuku ya Hijabu

Mahakama ya jimbo la St. Gallen nchini Uswisi imefuta hukumu ya kupiga marufuku kuvaa Hijabu msichana mmoja wa shule mwenye umri wa miaka 13 katika skuli moja iliyoko kaskazini mwa jimbo hilo.
Hakimu wa mahakama hiyo sambamba na kukubali mashtaka ya wakili wa mwanafunzi huyo Muislamu  kwamba uamuzi wa shule hiyo umekinzana na haki ya kuabudu kwa mujibu wa sheria ya kifederali ya Uswisi na pia Mkataba wa Haki za Binadamu, ameondoa marufuku ya Hijabu aliyokuwa amewekewa msichana huyo.

Hakimu wa kesi hiyo pia amesema, hakujathibitishwa ukiukwaji wowote wa sheria za shule uliosababishwa na kuvaa Hijabu msichana huyo.

 Inafaa kuashiria hapa kuwa, nchini Uswisi kuna Waislamu laki 4 ambao ni sawa na asilimia 5 ya wananchi milioni 8 wa nchi hiyo ya bara la Ulaya.

0 comments:

Post a Comment