Nov 15, 2014

“Kura ya Maoni iamue mustakabali wa Bahrain”

Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesema kuwa, kufanyika kura ya maoni kwa ajili ya kuainisha mustakbali wa Bahrain ndiko kutakodhamini haki muhimu za wananchi wa nchi hiyo. 
Ayatullah Muhammad-Ali Movahedi Kermani sambamba na kuashiria kufanyika uchaguzi wa Bunge la Bahrain Novemba 22 mwaka huu, amesema kuwa wananchi wa nchi hiyo watasusia uchaguzi wa kimaonesho na watashiriki tu kura ya maoni ya kuainisha mustakbali wa nchi yao ambayo inaungwa mkono pia na maulamaa wa Bahrain.

Ayatullah Muvahedi Kermani pia amelaani mashambulio ya askari wa Israel katika msikiti wa al Aqswa na kusema kuwa, kuendelea jinai za Wazayuni katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina kutapalekea kuanza Intifadha nyingine.

 Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran vilevile amegusia ripoti za Ahmad Shahid, Ripota Maalumu wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kuhusiana na Iran, na kusema kwamba kama Ahmad Shahid angekuwa anafuatilia kweli haki za binadamu, alipaswa kwenda Ukanda wa Gaza au Syria na kusikiliza wanawake na watoto wasio na hatia wa maeneo hayo wanaoishi katika hali ngumu kutokana na vitisho vya askari wa utawala ghasibu wa Israel na magaidi.

0 comments:

Post a Comment