Nov 15, 2014

Marufuku ya kuingia Masjidul Aqsa kuondolewa

Utawala wa Kizayuni wa Israel umesema kuwa utaruhusu Wapalestina wa marika yote kusali katika msikiti mtukufu wa al Aqswa, baada ya kupata mashinikizo kwa kuzuia Wapalestina wasiingie kwenye msikiti huo.

Msemaji wa Polisi ya Israel Mickey Rosenfeld amesema leo kuwa, hakutakuwa tena na kizuizi cha umri katika kuingia wafanyaibada wa Palestina katika msikiti wa al Aqswa, kwa mara ya kwanza baada ya miezi kadhaa. 

Hata hivyo ameongeza kwamba vikosi zaidi vya polisi vimepelekwa huko Mashariki mwa Quds mapema leo.

 Maafisa wa Israel wameeleza kwamba, marufuku hiyo imeondolewa kufuatia mazungumzo ya hivi karibuni kati ya Mfalme Abdullah II wa Jordan na Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu.

Kwa wiki kadhaa msikiti huo mtukufu kwa Waislamu duniani umegeuka kuwa sehemu ya makabiliano kati ya waumini wa Kipalestina, walowezi wa Kizayuni na askari wa utawala haramu wa Israel. 

 Machafuko yalianza mwezi uliopita baada ya Israel kuwazuia wanaume wenye umri wa chini ya miaka 50 kuingia kwenye msikiti huo, baada ya Mzayuni mwenye siasa kali Yehuda Glick kuuliwa na watu wasiojulikana.

0 comments:

Post a Comment