Watu wasiofahamika leo wameichoma
moto mahakama moja katika mji wa Alexandria nchini Misri.
Watu hao
wasiofahamika wamelichoma moto jengo la mahakama moja katika mji wa
Alexandria ikiwa ni kuendelea ghasia za wananchi baada ya kutolewa
uamuzi wa kumtoa hatiani dikteta Hosni Mubarak, dikteta wa zamani wa
Misri, wanawe wawili, Waziri wa Mambo ya Ndani wa wakati wa utawala wake
na manaibu wake kwa tuhuma zilizokuwa zikiwakabili za kuwaua wafanya
maandamano katika Mapinduzi ya wananchi ya mwezi Januari mwaka 2011.
Wakati huo huo mji wa Alexandria umeshuhudia milipuko miwili katika mahakama ya al Munshiya na katika klabu ya majaji katika mji huo na hivyo kusababisha kufungwa baadhi ya barabara.
Wakati huo huo mji wa Alexandria umeshuhudia milipuko miwili katika mahakama ya al Munshiya na katika klabu ya majaji katika mji huo na hivyo kusababisha kufungwa baadhi ya barabara.
Vikosi vya usalama vya Misri
jana iliwatia nguvuni baadhi ya watu waliokuwa na lengo la kuandamana
katika meidani ya at Tahrir ili kulalamikia uamuzi huo wa mahakama.
0 comments:
Post a Comment