Oct 2, 2014

Mashambulizi dhidi ya Daesh ni kisingizio tu cha US

Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, mashambulizi ya Marekani dhidi ya kundi la Daesh ni kisingizio tu cha kuangamiza miundombinu ya Syria.
Shirika la Habari la Fars limemnukuu Dk Ali Larijani akisema hayo leo wakati wa kufunga Maonyesho ya Tano ya Kitaifa ya Vitabu vya Kujihami Kutakatifu hapa mjini Tehran na kuongeza kuwa, Rais wa Marekani amedai kuwa ataliangamiza kabisa kundi la Daesh lakini ukweli wa mambo ni kuwa hayo ni madai tu yasiyo na ukweli, kwa uhakika wa mambo ni kwamba lengo la Marekani ni kuangamiza miundombinu ya Syria. Spika wa Bunge la Iran vile vile amewaambia viongozi wa nchi zinazoshirikiana na Marekani kwamba, lengo la Marekani ni kuzidi kuwa na ushawishi wa kijeshi nchini Iraq na kuwaweka madarakani vibaraka wake nchini Syria. 

Dk Larijani ameongeza kuwa, hatua ya Iran ya kujihami kiume katika vita vya miaka minane vilivyoanzishwa na utawala wa wakati huo wa Iraq imeathiri moja kwa moja matukio mengine katika eneo hili yakiwemo ya vita vya siku 33 na 22 vya Lebanon na Ghaza, na inabidi matukio ya wakati wa vita vya kujihami kutakatifu Iran yachunguzwe zaidi ili kuzidi kupata uzoefu wa kujilinda.

0 comments:

Post a Comment