Oct 3, 2014

Kiongozi wa upinzani nchini Burundi ahukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela

Léonce Ngendakumana, mwenyekiti wa muungano wa upinzani nchini Burundi ADC-Ikibiri,
Léonce Ngendakumana, mwenyekiti wa muungano wa upinzani nchini Burundi ADC-Ikibiri,
Esdras Ndikumana

Kiongozi wa muungano wa upinzani nchini Burundi wa ADC Ikibiri, Leonce Ngendakumana amehukumiwa kifungo cha mwaka moja jela. Akizungumza na shirika la habari la Ufaransa la AFP, leonce Ngendakumana amesema anatuhumiwa kwa kosa la mashtaka ya uongo dhidi ya chama tawala, na ameshutumu hukumu hiyo ambayo amesema ni ya kisiasa inakuja wakati huu Burundi ikielekea kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Ngendakumana amehukumiwa kwa ajili ya shutuma za uongo, kashfa na chuki ya kikabila kutokana na yaliyomo katika barua iliyotumwa Februari kwenye ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon, ambamo alikituhumu chama tawala nchini Burundi, CNDD -FDD kuandaa mpango kama ule uliondaliwa nchini Rwanda ambao mwisho wa siku uliishia kwenye mauaji ya kimbari mwaka 1994.

Leonce Ngendakumana ndiye kiongozi wa Muungano wa vyama vya upinzani nchini Burundi ADC/Ikibiri, mara kadhaa amekuwa akimemea serikali ya Burundi kutokana na kile anachodai hujma za serikali dhidi ya upinzani kwa kuwanyima haki ya kujieleza.

0 comments:

Post a Comment