MJUMBE WA HALMASHAURI KUU CCM TAIFA MHE DR NAJIM AKIZUNGUMZA NA WANACHAMA KATIKA MKUTANO MKUU WA CHAMA HICHO HAPO JANA.
Ahadi
ya kuwapatia Ardhi ya kutosha Umoja wa Maendeleo Wakaazi wa Mkoa wa Tanga Waishio
Dar es salaam (UMATADA) imetolewa.
Ahadi
hiyo imetolewa jana katika Mkutano Mkuu wa Chama hicho uliofanyika katika
viwanja vya Shule ya Al haramaini iliyopo Ilala Jijini Dar es salaam
Akitoa
ahadi hiyo Mjumbe wa Halmashauri kuu CCM Taifa Mhe Dr Najim amesema,”kuzungumzia
heka hamsini kwa chama kikubwa kama hiki ni fedheha ni muhimu tuwe na heka elfu
mbili”alisema kwa msisitizo mkubwa huku akishangiliwa na wajumbe
Aliendelea
kusema kwamba “nimevutiwa na yaliomo
katika risala yenu,kwa kuwa nami ni mwanachama na ni mdau wa maendeleo nina
ahidi nitatumia kila njia kuhakikisha nawapatia ardhi yenye ukubwa wa heka elfu
mbili na tutakapo kutana katika mkutano mkuu wa mwaka nitawafahamisha hatua
nitakayofikia”
Dr
Najim ambaye pia ni mkurugenzi wa
madaini Tanzania alimwakilisha Mgeni Rasmi Diwani wa kata kwematiku Mhe Bereko.
Awali
akisoma risala kwa niaba ya wajumbe,Al haj Abdallah Sabaya alisema Umoja wao
umebahatika kupata shamba katika kijiji cha Kwamsala lenye ukubwa wa heka Hamsini
lakini wameshindwa kuliendeleza kutokana na mgogoro.
Kupitia
risala hiyo aliutaja mgogoro huo kuwa ni madai ya kijiji cha komarasa kwamba
shamba hilo lipo ndani ya mipaka ya kijiji chao na kumuomba Mhe Diwani aingilie
kati mgogoro huo.
Aidha
kupitia mkutano huo Umoja huo ulizundua Vitambulisho maalumu ambapo Mhe Dr Najim
aliwakabidhi wanachama.
Umoja
huo ulioanzishwa mwaka 1999 hadi sasa una wanachama zaidi ya 275.
BAADHI YA WANACHAMA WAKIFUATILIA KWA MAKINI MKUTANO HUO.
VIONGOZI WA UMATADA WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MWAKILISHI WA MGENI RASMI MHE DR NAJIM
KATIBU WA SACCOS AKIWASILISHA TAARIFA ZA MAENDELEO YA SACCOS YA CHAMA HICHO.
AL HAJ ABDUL SABAYA AKISOMA RISALA KWA NIABA YA WAJUMBE
MHE DR NAJIM AKIMKABIDHI KITAMBULISHO MMOJA WA WANACHAMA WA UMATADA MUDA BAADA YA KUZINDUA VITAMBULISHO VYA UMATADA
0 comments:
Post a Comment