MWENYEKITI WA TAASISI YA AL MADINA SHEIKH ALLY MUBARAKAH AKIONGEA KATIKA SEMINA ILIYOFANYIKA JANA KATIKA UKUMBI WA AL HARAMAIN JIJINI DAR ES SALAAM
Kundi
la Mahujaji wapatao Mia sita linalo undwa kwa Ushirikiano wa Taasisi nane
linalojulikana G8 wameaswa kutokujihusiha na mambo yatakayopelekea kuharibu
Hijja zao.
Akizungumza
katika Semina ya mwisho kwa Mahujaji wa taasisi hizo,Mwenyekiti wa Taasisi ya
Al Madina Sheikh Ally Mubarakah amesema ni vyema kwa Mahujaji wakifika katika
viwanja vitukufu kufanya ibada pekee kwani ndicho walicho kisumbukia.
Aliwaasa
mahujaji kwamba wasiwe na tabia ya kudadisi au kusema juu ya tofauti ya huduma
baina ya kundi na kundi.
“Ndugu
zangu mahujaji watarajiwa,kwa uwezio wa Allah tuna kwenda Makkah basi
tujiepushe na mambo ambayo hayana msingi wala faida”alisema
Aliendelea
kusema kwamba “utakuta watu wanasema kundi au taasisi Fulani imekula chakula
kizuri au imelala hotel mzuri,ndugu zangu haya siyo yaliyotupeleka”
Semina
hiyo ilifanyika jana katika ukumbi wa Al haramain uliopo Jijini Dar e salaam.
G8
inaundwa na Taasisi za Al madina,Ummul Quraa,Tabazat Baabu salaam,Markaz
Shamsiyyah,Ahlul Baytu,East Afrika Hajj Trust,Islamic Development Centre na Daarul Hadiith.
G8
Litaondoka tarehe 23,24 na 26 mwezi huu In Shaa Allah.
Munira
blog inawatakia safari njema na HIJJA MABROUL
NAIBU KADHI MKUU WA TANZANIA AL HAJ SHEIKH ABOUBAKRI ZUBEIR AKIZUNGUMZA KATIKA SEMINA HIYO.
BAADHI YA MAHUJAJI WAKIWA KATIKA SEMINA YA MWISHO ILIYOFANYIKA JANA
BAADHI YA MAHUJAJI WAKIWA KATIKA SEMINA YA MWISHO ILIYOFANYIKA JANA
0 comments:
Post a Comment