Sep 11, 2013

Wasusia Rasimu ya Katiba kwa kukosa Posho



MKUTANO wa kujadili Rasimu ya Katiba Mpya ulioandaliwa na Chama cha Wasioona wilayani Kahama umevunjika baada ya washiriki kususia wakidai posho.

Mkutano huo ulivunjika siku ya pili baada ya wajumbe hao kutoka asasi mbalimbali zisizokuwa za kiserikali wakiongozwa na baadhi kutoka kwa Chama cha Walemavu wa Macho na Viungo, kukataa kuhudhuria mkutano huo hadi Ofisa wa Ruzuku wa The Civil for Foundation Society, Ghati Horombe, kutangaza kuwalipa posho hizo.
Tangazo la ofisa huyo liliongeza idadi ya washiriki kwa siku ya tatu jambo lililomfanya Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu wilayani Kahama, Maico Nkanjiwa aliwaonya kuacha tabia ya kutanguliza maslahi katika masuala ya kujadili maisha yao.
Siku ya kwanza wajumbe zaidi ya 100 walihudhuria baada ya Nkanjiwa kuwatangazia kuwa kusingelikuwa na posho isipokuwa wangelipata chai na chakula cha mchana; jambo hilo lilizusha mzozo kwa washiriki hao wakidai wasingeliwezi kushindia chakula.
Walisema wasingeliweza kula chakula huku familia zao zikiadhirika kwa kushinda na njaa majumbani mwao na kudai kuwa ni vema wangeondoa gharama za chakula, badala yake kuwalipa pesa, kuliko kuwashindisha hapo bila malipo.
Kwa upande wake Horombe aliwataka Watanzania kuacha tabia hiyo kwa kuwa inaleta sura mbaya kwa wafadhili.
Hata hivyo mkutano huo ulimalizika kwa washiriki kuunga mkono uwepo wa serikali tatu kwa madai kwamba serikali mbili haina maslahi kwa Watanzania.

0 comments:

Post a Comment