Feb 22, 2015

Rais aliyejiuzulu Yemen akimbilia eneo la Aden

Abd Rabbu Mansour Hadi, Rais aliyejiuzulu nchini Yemen ametoroka kutoka mji mkuu Sana'a na kukimbilia katika mji wa bandari wa Aden baada ya kuwa chini ya kifungo cha nyumbani kwa majuma kadhaa.
 
Watu wa karibu naye wanasema Hadi ametoroka kutoka nyumbani kwake alikokuwa akizuiliwa na wapiganaji wa harakati ya Ansarullah na ameelekea katika mji wa Aden ulioko kusini mwa Yemen.

Januari 22, Hadi alitangaza kujiuzulu pamoja na serikali ya Waziri Mkuu, Khalid Bahah baada ya kushitadi mgogoro nchini humo.

 Wachambuzi wengi wanasema rais wa zamani wa Yemen ameamua kukimbilia mjini Aden kwa kuwa ndiko anakoungwa mkono zaidi na wazee wa kikabila wa mji huo. 

Baadhi ya duru zinaarifu kuwa, kiongozi huyo aliyejiuzulu anapanga kwenda Saudi Arabia au Marekani kutokana na kuendelea kudhoofu afya yake.

0 comments:

Post a Comment