Dec 2, 2014

Shambulio la kigaidi laua nchini Kenya

Askari wakiwa katika eneo la tukio mojawapo la mashambulio ya kigaidi nchini Kenya
Mtu mmoja ameripotiwa kuuawa nchini Kenya kufuatia mlipuko katika klabu moja ya usiku katika mji wa Wajir kaskazini mwa Kenya.

Kwa mujibu wa Kamishna wa Polisi wa Wajir, Frederick Sishia, shambulio hilo limefanyika saa mbili usiku na kuua mtu mmoja na watu wengine wanne wamejeruhiwa.

Washambuliaji hao walitumia magruneti na silaha nyingine za kijeshi kufanya shambulio hilo.

Wiki iliyopita watu wengi waliuawa eneo la Mandera kaskazini mwa Kenya.

Kenya imejikuta ikilengwa na mashambulio ya kigaidi tangu majeshi yake yapelekwe nchini Somalia kukabiliana na wapiganaji wa Al Shabab. 

Mbali na miji ya kaskazini mwa Kenya kushambuliwa kila mara, miji mikubwa nchini humo ya Nairobi na Mombasa imekuwa ikilengwa na mashambulio ya kigaidi.

0 comments:

Post a Comment