Waislamu nchini Kenya wamelalamikia hatua ya polisi ya
nchi hiyo ya kufunga misikiti kadhaa katika Kaunti ya Mombasa.
Waislamu
wa nchi hiyo wamevitaka vyombo vya usalama vya Kenya kufungua misikiti
ya Mussa, Swafa, Mina na Sakina ambayo ilifungwa hivi karibuni na polisi
kwa sababu za kiusalama.
Viongozi wa Kiislamu nchini Kenya wanaikosoa
vikali hatua hiyo ya polisi ya Kenya ya kufunga misikiti hiyo wakisema
hilo sio suluhisho la kupambana na ugaidi.
Juma lililopita polisi ya
Kenya ilivamia misikiti kadhaa katika Kaunti ya Mombasa na kuwatia
mbaroni mamia ya vijana wa Kiislamu ikiwatuhumu kwa ugaidi.
Polisi ya
Kenya imetangaza kuwa, ilipata silaha katika misikiti hiyo, madai ambayo
yanatiliwa shaka na baadhi ya Waislamu wa nchi hiyo.
Aidha viongozi wa
Kiislamu nchini Kenya wanapinga vikali hatua ya polisi ya kufunga
misikiti hiyo na kusisitiza kwamba, Waislamu wa nchi hiyo wamekuwa
wakiandamwa katika vita dhidi ya ugaidi.
Katika upande mwingine Wabunge
wa Kenya katika mji mkuu Nairobi wameeleza masikitiko yao kutokana na
kutokuwa na matunda hatua za kuimarisha usalama na kutahadharisha
kwamba, kufungwa misikiti minne ya Mussa, Sakina, Swafa na Mina huko
Mombasa ni kinyume cha kisheria na wametaka kuhitimishwa suala hilo.
0 comments:
Post a Comment