Oct 1, 2014

WALIOBAKWA WALALAMIKIA NDOA ZA MKEKA

Waliobakwa na kisha kuozwa waume katika wilaya ya Wete mkoa wa kaskazini Pemba, wamesema ndoa za mkeka zinazofungwa kama sulhu, zinachangia kwa kiasi kikubwa kasi ubakaji katika jamii.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi, umeonesha jamii imekuwa na uharaka wa kuwafungisha ndoa mara wanapobaini kuwepo vitendo hivyo,wakidhani ndio sulhu ya kuvitokomeza badala yake vimekuwa vikichangia kuongezeka.

Uchunguzi umebaini imekuwa na kawaida kuharakia sulhu ya ndoa, hata kama shauri hilo limeshafikishwa katika vyombo vya sheria, jambo ambalo huwapa jeuri na kiburi wabakaji.

Mmoja kati ya waathirika wa ubakaji na kisha kuolewa mwenye miaka 17, mkaazi wa shehia ya Mchangamdogo wilayani humo, alisema binafsi baada ya kujihisi ameshapewa ujauzito, alikimbilia kituo cha polisi na kisha muhusika kukamatwa.

Awali, alimueleza mpenzi wake huyo kwamba, ameshampa ujauzito na alipokataa, ndipo alichukua uamuzi wa kukimbilia kituo cha polisi Wete,inagwa kesi hiyo haikufikishwa mahakamani.

0 comments:

Post a Comment