Oct 1, 2014

Seli za mateso za chini ya ardhi zagunduliwa Yemen

Kundi la watetezi wa haki za binadamu wa Yemen na waandishi wa habari wamegundua njia za chini kwa chini na seli za wafungwa zilizo kinyume cha sheria huko San'aa mji mkuu wa nchi hiyo.
Seli na njia hizo za chini ya ardhi zimegunduliwa ndani ya kituo cha kijeshi ambacho kilikuwa kikisimamiwa na Meja Jenerali mtoro Ali Mohsen al Ahmar, kaka wa kambo wa dikteta wa zamani wa Yemen Ali Abdullah Saleh.

Abdurahman Abdul-wahid, afisa wa kituo cha haki za raia cha Yemen amesema kuwa seli hizo walizozikuta chini ya ardhi zipo katika hali ya kutisha na kwamba wamepata pia baadhi ya minyororo ambayo ilikuwa ikitumika kutesea watu. 

Itakumbukwa kuwa wapiganaji wa harakati ya Ansarullah walikidhibiti kituo hicho cha kijeshi baada ya kujiri mapigano makali huko San'aa kati yao na vikosi vitiifu kwa Meja Jenerali mtoro Ali Mohsen al Ahmar.  

0 comments:

Post a Comment