Oct 1, 2014

MANSOOR AOMBA AKATIBIWE NJE YA NCHI

WAZIRI wa zamani wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ)
Mansour Yussuf Himid anayekabiliwa na kesi ya kupatikana na silaha ya moto na risasi 407 amewasilisha maombi matatu mahakamani ikiwemo kuruhusiwa kusafiri  nje ya nchi kuanzia Oktoba 22 mwaka huu, imefahamika Visiwani humo jana.
Maombi hayo yamewasilishwa na Wakili wake Samah Salaha mbele ya Hakimu wa Mahkama ya Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Khamis Ramadhan Abdalla, akitaka mteja wake hapatiwe ruhusa ya kwenda kufanyiwa uchunguzi wa afya yake nchini India pamoja na kufanyiwa mazoezi ya viungo vya magoti nchini Ujerumani.
Samah alisema kwamba Mansour amekuwa akifanyiwa uchunguzi wa afya yake kila mwaka nchini India na kuomba mahakama kuondoa mashariti ya dhamana yake ya kutosafiri nje ya nchi kama ilivyokuwa imeamuliwa na Jaji Abraham Mwampashi Agositi m18 mwaka huu.
:Naomba kuwasilisha maombi ya mteja wangu anataka kusafiri nje ya nchi kuanzia Oktoba 22 hadi Novemba 12 nchini India na Ujerumani kuchunguza afya yake na kufanya mazoezi ya viungo vya magoti nchini Ujerumani:alisema Samah.
Alisema kutokana na mazingira hayo pia mteja wake apewe hati ya kusafiria pamoja na kuruhusiwa kusafiri kati ya Zanzibar na Dar es salaam kutokana na shughuli zake za kibiashara na kifamilia.
Mwanasheria huyo alisema kwakuwa Mama yake Masour baadhi ya wakati analazimika kufuata matibabu Tanzania bara vizuri mteja wake akapunguziwa mashariti ili hapate nafasi ya kumuhudumia mama yake hasa kwa kuzingati yeye ndiyo Mtoto mkubwa wa Kiume katika familia yao.
Hata hivyo Mwendesha mashtaka wa Serikali Ally Yussuf Mohamed alisema kwamba upande wa mashtaka hauna pingamizi kama mshtakiwa hataweza kuwasilisha nyaraka za kuthibitisha kama amekuwa akitibiwa nje ya nchi kila mwaka kwa kuwasilisha nyaraka pamoja na nyaraka za biashara anazofanya kati ya Zanzibar na Tanzania bara.
Upande wake Hakimu Khamis Rmadhani Abdalla, alimtaka mshtakiwa kuwasilisha nyaraka hizo zikiwa katika mpangilio wa kisheria pamoja na maombi yake
Waziri huyo wa zamani amefunguliwa mashtaka baada ya kupekuliwa nyumbani kwake Chukwani Zanzibar na kukamatwa na silaha ya moto aina ya bastola na risasi 407 kinyume na sheria na yupo nje kwa dhamana ya mashariti ya kutosafiri bila ya ruhusa ya mahakama, fedha taslimu Milioni tatu, wadhamini wawili wenye bondi ya shilingi milioni tano kila mmoja na hati ya kusafiria kushikiliwa na Mahakama
Kuhusu kesi ya msingi Mwansheria wa SMZ Ally Yussuf Mohamed alisema kwamba upelelezi wake bado kukamilika lakini kwa mujibu wa sheria ndani ya miezi tisa utakuwa umekamilika na kutoa nafasi kesi kuanza kusikilizwa kabla ya kutolewa hukumu.

0 comments:

Post a Comment