WATOTO sita,
wakiwemo wawili wa kiume wenye umri wa miaka 8 hadi 14 wameharibiwa
vibaya sehemu zao za siri baada ya kubakwa kanisani na watu wanaodaiwa
ni wachungaji.
Wakiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru walikopelekwa kwa
matibabu na kuangaliwa maambukizi ya magonjwa ya zinaa, watoto hao
walidai kufanyiwa mchezo huo kwa nyakati tofauti na wachungaji watatu
wa kanisa hilo lililopo eneo la Feed Force, Kwamorombo jijini Arusha.
Mmoja wa watoto hao anayesoma darasa la 4 katika shule ya msingi
alieleza kuwa yeye na wenzake wamekuwa wakifanyiwa mchezo mchafu katika
kanisa hilo baada ya wachungaji hao kuwapatia shilingi 2,000 za kufungia
mdomo.
“Siku moja nilipofika shuleni wenzangu wakaniambia niende pale kanisani
tukapewe hela, nilipofika niliwaona wenzangu wengine wakifanyiwa mchezo
mchafu na mimi mchungaji aliniambia niiname akanifanyia kitendo kibaya
na kunipa shilingi 2,000, niliumia sana,’’ alisema mwanafunzi mmoja.
Mwanafunzi mwingine alisema amekuwa akitoroka shuleni na wenzake na kwenda kwa watumishi hao ambapo huwaingiza katika kanisa hilo na kujifanya wanawaombea baadaye huwafanyia mchezo mbaya.
“Tukifika huwa wanatufungia ndani na kutuambia tuwanyonye, baadaye
wanatubaka na wakimaliza wanatuambia tukisema kwa mtu yeyote
watatuchinja na kutuzika ndani ya kanisa lao,” alisema denti huyo.
Wanafunzi hao walieleza kuwa watumishi hao huwarubuni kwa kuwaeleza kuwa
watawasaidia kuwasomesha iwapo watakuwa wakienda kwenye kanisa hilo na
kuwaingilia.
Mzazi mmoja wa watoto hao, Julius, mkazi wa Kwamorombo alisema mtoto wake alimweleza kwamba amekuwa akifanyiwa mchezo mbaya na watumishi hao baada ya kupewa shilingi 2,000.
Mzazi mmoja wa watoto hao, Julius, mkazi wa Kwamorombo alisema mtoto wake alimweleza kwamba amekuwa akifanyiwa mchezo mbaya na watumishi hao baada ya kupewa shilingi 2,000.
Alisema aligundua hilo kufuatia tabia ya mtoto wake kuchelewa kurudi nyumbani.
Naye Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chadema, Godbless Lema ambaye
alifika hospitalini kuwajulia hali watoto hao alisikitishwa na kitendo
hicho na kulitaka jeshi la polisi lifanye uchunguzi wa kina kwa
kushirikiana na vipimo vya kidaktari ili kupata ukweli wa tukio hilo.
“Nimeongea na mkuu wa mkoa, Magesa Mulongo ambaye ameahidi kulifuatilia
kwa kina suala hili na kujua undani wake,’’ alisema Lema.
Hata hivyo, watoto hao baadaye walihamishiwa katika Hospitali ya Seliani
kwa ajili ya vipimo zaidi huku taarifa za awali zikithibitishwa na
daktari wa hospitali hiyo kuwa, baadhi yao walikutwa na michubuko na
kupanuka sehemu za siri hali inayooneshwa kuingiliwa.
Watuhumiwa wa tukio hilo wanashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi
jijini hapa kwa uchunguzi zaidi na Kamanda wa Polisi Arusha, Leberatus
Sabas amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
0 comments:
Post a Comment