Sep 30, 2014

Maalim- Awataka Wawekezaji na Wafanyabiashara Kutumia Fursa katika Uwekezaji Afrika. Mashariki

 Mhe. Maalim Seif akimsikiliza kijana wa miaka 22 ambaye amepewa heshima kubwa ya ubunifu wakati wa mijadala kwenye mkutano mkuu wa Uchumi wa Dunia (WEF) nchini Uturuki.
 
Na Khamis Haji, Istanbul                                    
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad amesema hali ya amani na utulivu katika eneo la Afrika Mashariki ni ya kuridhisha na wawekezaji vitegauchumi pamoja na wafanyabiashara wanaotaka kutumia fursa zilizopo katika eneo hilo waje na waondowe hofu.

Maalim Seif ameyasema hayo katika mkutano wa Uchumi wa Dunia (WEF) unaoendelea katika jiji la Istanbul nchini Uturuki alipotakiwa kutoa maoni yake juu ya hali ya usalama katika eneo hilo la Afrika Mashariki.

Amesema iliwahi kujitokeza hali ya kukithiri vitendo vya kiharamia vilivyo sababishwa na kukosekana utulivu katika nchi ya Somalia, lakini matukio hayo hivi sasa yamepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na mashirikiano ya pamoja kati ya nchi zilizopo jirani pamoja na Jumuiya ya Kimataifa.

Amesema nguvu hizo za jumuiya ya kimataifa zinapaswa kuendelezwa, ikiwemo kuzijengea uwezo nchi za Afrika katika kukuza upatikanaji wa ajira kwa vijana, ili kuwaepusha na uwezekano wa kushawishiwa na makundi ya watu waovu ambayo yamekuwa chanzo cha kuongezeka matendo maovu.

“Hali katika eneo la Afrika Mashariki ni salama sana kuna vivutio vya kila aina,  wawekezaji tumieni fursa hii kuja kufungua miradi yenu”, amesema Maalim Seif.
Amesema ni jukumu la Jumuiya ya Kimataifa kuzipa msukumo nchi zenye matatizo ya uchumi, likiwemo tatizo kubwa la uhaba wa ajira miongoni mwa vijana, ambalo litawaepusha vijana  na tabia ya kurubuniwa kuingia katika matendo yasiofaa.

Maalim Seif Ahudhuriwa Mkutano wa Kimataifa wa Uchumi Uturuki.

  1. Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan akijiandaa kuhutubia mkutano wa Dunia wa Uchumi, ambapo amezilaumu baadhi ya nchi za Magharibi, ikiwemo Marekani kutokana na sera zao nchini Irak na Syria.
Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar wa Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad akiwa na Waziri Mkuu wa Mali, Mhe. Moussa Mara (kulia) na viongozi wengine wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Uchumi wa Dunia, jijini Istanbul, Uturuki.

 Mh. Maalim Seif akibadilishana mawazo na Afisa katika Serikali ya Uturuki wakati wa mkutano wa Uchumi wa Dunia (WEF). 
Mhe.Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad,akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Italia, ambaye pia anahusika na Uturuki, James Msekela wakati wa mkutano mkuu.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Maalim Seif akitoka kwenye mkutano wa WEF. Kushoto kwake askari wa Uturuki akimhakikishia ulinzi.
Wataalamu mbali mbali katika masuala ya Ubunifu na Ujasiri Amali, wakiwemo kutoka Israel, Marekani na Ujerumani waliofika katika mkutano wa WEF baada ya kuwasilisha mada zao. Mjadala wa mada hizo ulimhusisha Mhe. Maalim Seif.

0 comments:

Post a Comment