KATIKA hali ya kushangaza, mtu mmoja ambaye ni fundi seremala aitwaye
Emmanuel Carlos, mkazi wa Kwabinyau Magomeni jijini Dar amekutwa akiwa
amejinyonga saa mbili asubuhi Septemba 23, mwaka huu katika kile
kinachodaiwa kuchoshwa na mgogoro wa kifamilia.
Baadhi ya majirani wa eneo hilo walisema kutokana na ugomvi huo, marehemu alikuwa akirudi nyumbani usiku akiwa amelewa na kumtukana matusi mkewe huku baadhi wakienda mbali na kudai alikuwa haachi hela ya matumizi.
Hata hivyo, mkewe marehemu anadaiwa kuwa na biashara yake ya samaki na alikuwa akijituma ili kuhakikisha anapata nauli ili arejee nyumbani kwao.

Akizungumza na waandishi wetu Mariamu alisema kuwa siku moja kabla ya tukio, mumewe alirudi nyumbani na kumtukana huku akilia na kumwambia kuwa atamkumbuka sana katika maisha yake na kwamba kabla ya kupambazuka mmoja wao atakuwa amekufa.
“Siku iliyofuata alipoamka alinikuta naosha vyombo, akanitazama kwa jicho baya kisha akaenda chumbani kwake ambako alijifungia.
Naye mjumbe wa serikali ya mtaa huo, Jumanne Mneka alikiri kufahamu mgogoro wa familia hiyo na kusema walikuwa wakiwasuluhisha kila mara.
Majirani wakiwa wameshtushwa na kushangazwa na jambo hilo, waliungana na wapita njia kwenda kushuhudia tukio hilo, hali iliyoufanya mtaa huo usipitike kwa muda.
Waandishi wetu waliwashuhudia polisi wakifika eneo hilo na kuuchukua mwili na kuupeleka katika Hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya uchunguzi.
Marehemu ameacha mke na watoto wawili
Habari hizi kwa hisani ya GP
0 comments:
Post a Comment