Wakati Rais Jakaya
Kikwete akikutana na viongozi wa vyama vya siasa vinavyounda Kituo cha
Demokrasia Tanzania (TCD) ili kuzungumzia mchakato wa Katiba, Jukwaa la
Wakristo Tanzania (TCF), limesema amani ya nchi iko mikononi mwa
kiongozi huyo mkuu wa nchi.
Kwa maana hiyo viongozi wa vyama vya siasa hasa
vile vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wanatarajiwa
kusafiri hadi Dodoma kumfuata Rais Kikwete ambaye leo anaingia katika
siku ya tatu ya ziara yake mkoani hapa, iliyoanza juzi katika Wilaya ya
Kongwa.
Baadhi ya viongozi ambao wanatarajiwa kushiriki
mkutano huo ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Mwenyekiti wa
Chadema, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na
Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia.
Pia katika orodha hiyo wamo Mwenyekiti wa TCD
ambaye pia ni Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo, Mwenyekiti wa TLP,
Augustine Mrema na mwakilishi wa vyama visivyo na wabunge ndani ya TCD
ambaye pia ni Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa.
Ukiondoa Kinana, viongozi wengine ni wajumbe wa Bunge Maalumu.
Ukiondoa Kinana, viongozi wengine ni wajumbe wa Bunge Maalumu.
Habari zilizopatikana juzi na jana Dar es Salaam
na Dodoma na kuthibitishwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salva
Rweyemamu zinasema mkutano huo umepangwa kufanyika leo jioni baada ya
Rais Kikwete kuhitimisha ziara yake katika Wilaya ya Chamwino na unaweza
kuendelea hadi usiku kutokana na jinsi ratiba ilivyokaa.
“Mkutano utafanyika hapa Dodoma katika muda wa
saa 48 kuanzia sasa na Rais hatakutana na Ukawa kama ambavyo imekuwa
ikidaiwa, anakutana na viongozi wa vyama vya siasa,”
Mwanzoni mwa wiki hii, Cheyo aliwaambia waandishi
wa habari mjini Dodoma kuwa Rais Kikwete alikuwa amekubali kukutana na
viongozi wa vyama vya siasa wiki hii ili kuzungumzia mustakabali wa
Katiba.
Hata hivyo, alipoulizwa jana siku ya mkutano pamoja na mahali utakapofanyika, Cheyo hakuwa tayari kuzungumza chochote.
Hata hivyo, alipoulizwa jana siku ya mkutano pamoja na mahali utakapofanyika, Cheyo hakuwa tayari kuzungumza chochote.
Mkutano huo wa Rais na viongozi hao umekuja
wakati ambao kamati za Bunge Maalumu zimekamilisha uchambuzi wa Rasimu
ya Katiba, bila kuwapo kwa wenzao wanaokaribia 120 ambao walisusia
mchakato huo tangu Aprili 16, kutokana na kile walichodai kuwa ni
kutoridhishwa na mambo yanavyokwenda.
Mara kadhaa Ukawa wamesisitiza kwamba kamwe
hawatarejea bungeni hadi pale masharti yao yatakapotekelezwa na CCM
kikishikilia msimamo wake kwamba masuala yote yanayohusu Katiba Mpya
lazima yatatuliwe ndani ya Bunge.
Kwa kuzingatia mazingira hayo ni dhahiri kwamba matokeo ya kikao hicho yanasubiriwa kwa shauku kubwa kwani yanaweza kusaidia kukwamua mchakato wa Katiba ambao umekosa uhalali wa kisiasa kutokana na Ukawa kuususia.
Kwa kuzingatia mazingira hayo ni dhahiri kwamba matokeo ya kikao hicho yanasubiriwa kwa shauku kubwa kwani yanaweza kusaidia kukwamua mchakato wa Katiba ambao umekosa uhalali wa kisiasa kutokana na Ukawa kuususia.
Mzigo wa amani
Wakati hayo yakiendelea Jukwaa la Wakristo
Tanzania (TCF) limetoa tamko kali kuhusu mchakato wa Katiba, na likiweka
bayana kwamba ni Rais Kikwete pekee ambaye anaweza kukwamua suala hilo.
Jukwaa hilo linajumuisha taasisi kubwa za
madhehebu ya Kikristo ambazo ni Baraza la Maaskofu Katoliki nchini
(TEC), Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Baraza la Makanisa ya
Kipentekoste Tanzania (CPCT) na Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA.)
0 comments:
Post a Comment