Jan 23, 2014

Maoni ya Maulamaa kuhusu Umoja wa Kiislamu

Mkutano wa Kimataifa wa Mkutano wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu ulifanyika Tehran kuanzia tarehe 17 hadi 19 Januari kwa mnasaba wa maadhimisho ya Maulidi ya Mtume Muhammad SAW na Imam Jaafar Sadiq AS. 

Kaulimbiu ya mkutano wa mwaka huu ilikuwa "Qur'ani na Nafasi Yake katika Umoja wa Umma wa Kiislamu". 

Mkutano huo ulioandaliwa na Jumuiya ya Kukurubisha Pamoja Madhehebu za Kiislamu uliwaleta pamoja wasomi, maualmaa na wanazuoni zaidi ya 300 kutoka nchi 50 za dunia. 

Kutoka Kenya washiriki walikuwa ni Kadhi Mkuu wa zamani Sheikh Hammad Qasim na Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu Kenya SUPKEM Profesa Abdulghafur el Busaidi. 

Mubarak Henia alipata fursa ya kuwahoji ili kupata maoni yao kuhusu Umoja wa Kiislamu.
Bonyeza hapa chini kuyasikiliza mahojiano hayo..

0 comments:

Post a Comment