Sep 20, 2013

Mimi si Msanii,Sihitaji malumbano-Mufti Simba



MUFTI wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), Issa Shaban bin Simba amesema yeye si msanii kama anavyoshutumiwa na Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Mazungumzo kati ya Waislamu na Serikali, Sheikh Suleiman Kilemile.
Mufti Simba alisema shutuma anazotupiwa zinatokana na malalamiko yake kwa Serikali kuhusu kupuuzia suala la Mahakama ya Kadhi.

Kutokana na hali hiyo, Mufti Simba alisema yeye yupo sahihi na kwamba anayemshutumu atumie sheria badala ya kulalamika kwenye vyombo vya habari.

Simba alisema anachofahamu ni kwamba kupatikana kwa Kadhi hakuhitaji ushirikishwaji wa taasisi zote za Kiislamu na kubainisha kuwa kama kuna kosa lililofanyika sheria ndiyo itatengua kitendawili hicho na si malalamiko.

“Huyo Sheikh Kilemile kama anadhani kulalamika ni dawa waulizwe Waislamu kuhusu Mahakama ya Kadhi na mimi sitaki kuendeleza mvutano kwenye vyombo vya habari,” aling’aka Mufti Simba.

0 comments:

Post a Comment