Aug 8, 2013

Swala ya Idd el fitri



MATAIFA 70 WASWALI IDD LEO,

  • AFRIKA KUSWALI KESHO PAMOJA OMAN.
  • NCHI YA NAIJA,INDIA NA INDONESIA ZA SWALI JANA.

Na mwandishi wetu wa munira.
Imeelezwa kwamba leo nchi sabini zimeswali swala ya iddil fitri baada ya kumaliza ibada ya funga ya Ramadhan.

Hayo yameelezwa na Katibu mkuu wa jopo la Masheikh na Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania Sheikh Khamis Mataka alipokuwa anazungumza katika kipindi cha Ramadhan kareem kinachoendeshwa na Sheikh Muhammad Idd kupitia luninga ya Channel Ten.

Ingawa imepishana na mahesabu ya falaq lakini nchi ya NAIJA,INDIA katika mji wa kirara na INDONESIA leo (Kwa maana jana tarehe 07/08/2013) wameswali Swala ya Idd”,alisema.

“Kwa nchi ya Saudi Arabia wao wataswali kesho (kwa maana leo) japo mamlaka ya Saud Arabia iliwatangazia waumini wake jana (kwa maana juzi tarehe 06/08/2013) waangalie mwezi ingawa wao hiyo juzi ilikuwa ni mwezi ishirini na nane”,mwisho wa kumnukuu.

Aliendelea kusema kwamba katika mataifa 70 yatakayo swali kesho (kwa maana leo) yamegawaniyika katika makundi matatu,kundi la kwanza ni kundi lenye mataifa 17 ambao walianza kufunga jumanne ya tarehe 9,kundi la pili la nchi 41 ni la wanaoifuata Saudia Arabia na kundi la tatu ni nchi ya Uturuki ambao wao wanafunga kwa mahesabu na sio kuuona mwezi.

Nimeshangazwa kuona kwamba ikiwa ni kweli madai ya unapoonekana mwezi katika nchi moja basi wanalazimika watu wa mataifa mengine kufunga,mbona leo (jana) nchi ya JAINA na baadhi ya miji katika inchi ya INDIA na INDONESIA wameswali Iddi kwa madai wameuona mwezi na Saudi Arabia hawakuswali,lakini kinachonishangaza zaidi iweje jana (juzi) mamlaka ya Saudii Arabia iliwatangazia waumini wake wautazame mwezi ilhali ni mwezi ishirini na nane,alihoji Sheikh mataka huku akiiweka wazi web site yenye kubainisha hayo kuwa ni “www,moonsiting.com”

Kwa upande wake msomi mashuhuri nchi ambaye pia ni mhadhiri wa chuo kikuu morogoro Sheikh Muhammad Abdul rahman Dedesi akichangia katika kipindi hicho alisema,”si muhimu mimi na wewe kujuwa lini mwezi umeandama,kwa mujibu wa sheria za kifiqihi jukumu hilo ni la kamati au mabaraza ya mwezi,shekh Muhammad nikwambie jambo la msingi,mwezi hautangazwi na radio au kituo cha televishen,mwezi unatangazwa na mamlaka ya kufuatilia mwezi katika taifa husika na waumini wa taifa hilo wanapaswa kufuata na kutekeleza maelekezo ya mamlaka ya kufuatilia na kuutangaza mwezi katika taifa husika,hebu nikupe mfano,leo wewe unaswali katika msikti wa Qiblaten pale kariakoo,upo ndani ya swala unamsikia Suddays anaswalisha katika msikiti wa mtoro anasema ALLAHU AKBAR anarukui,utamfuata huyo Suddays au utamfuata imamu anaye kuswalisha hapo Qiblaten”mwisho wa kumnukuu.

Katika hali ya kukinaisha maelezo,alitoa mfano mwengine ,”ikiwa umemuoa mwananmke,basi atalazimika kusikiliza na kufuata maelekezo yako na wala halazimiki kusikiliza wala kufuata maelekezo ya mume wa jirani yako”alisema.

Alikhitimsha kwa kusema kwamba “Baraza la kifiqihi la kiislamu ulimwenguni lilikaa na kutoka na maamuzi ambayo naomba niwasomee,kwamba suala la kuuthibitisha mwezi muandamo liachwe kwa mamlaka ya ofisi ya kadhi au mufti wa kila nchi husika”.mwisho wa kumnukuu sheikh dedesi.

Awali akizungumza kwa niaba ya Mufti wa Tanzania,Sheikh wa mkoa wa Dar es salaam Alhad Mussa Salum alisema wamewasiliana na watendaji wao kutoka katika vitongoji mbalimbali na kuwasiliana na makadhi na mufti wa nchi za Afrika mashariki na kujiridhisha kwamba mwezi haujaandama na hivyo waislamu wanawajibika kufunga kwa kukamilisha idadi ya siku thelathin.

SHEIKH KHAMIS MATAKA KATIBU MKUU WA JOPO LA MASHEIKH NA WANAZUONI WA KIISLAMU WA TANZANIA,AKIONGEA KATIKA KIPINDI CHA 39 CHA RAMADHAN KAREEM KILICHORUSHWA LIVE JANA KUPITIA LUNINGA YA CHANNEL TEN