Hivi ndio alivyopokelewa Mansour Yusuf Himid katika
Mkutano wa Kamati ya Maridhiano hapo Bwawani.
Umati mkubwa wa Wazanzibar wamefurika katika ukumbi wa
Bwawan Hall kufuatilia mjadala utakaoendeshwa na Kamati ya Maridhano juu ya
mustakbali wa Zanzibar.
Kwa mujibu wa mpashaji wetu ni kwamba muda huu Bwawan Hall limeshasheheni wengi wakiwa na shauku
kutaka kujuwa hasa kufuatia kufukuzwa uanachama katika chama chake mmoja wa
wajumbe wa kamati hiyo. Huyo ni Bw Mansour Yussuf Himid ambaye hivi karibuni
Chama cha Mapinduzi kulimfukuza uanachama. Uamuzi ambao wengi waliona
haukustahiki kwa vile ni haki yake kisheria kutoa maoni juu ya katiba mpya kama vile mwenyewe anavyoona.
MANSUOR YUSUPH HIMID,KADA ALIYEVULIWA UANACHA WA CCM.
Aidha wakati huo huo Mwanaharakati Maarufu Bw Mohamed Riami (Eddy Riami) ametangaza kujiondoa
katika Chama Cha Mapinduzi.
Akizungumza katika Kongamano lililotayarishwa na Kamati ya Maridhiano, hii
ilikuwa strong speech iliyowahi kutolewa na Bw Eddy Riami amesema yeye sio
mwanasiasa, akiwafananisha na Jusa na Mzee Moyo. Bali yeye ni raia kama walivyo raia wengine.
Amewataka Wazanzibar kujitolea kutafuta heshma zao na nchi yao. Alisema kwamba ni wao ndio waliompigia
kura Rais kwani Rais mwenyewe hakupiga kura katika uchaguzi uliopita. Hivyo
anajuwa vipi Zanzibar
itashinda kabla ya mwaka 2015. Alikuwa akikariri moja ya hotuba ya Mzee Karume
alpokuwa anakadiria kuwa Zanzibar
haihitaji uchaguzi
hadi baada ya miaka 50.
hadi baada ya miaka 50.
Ametaka suala la siasa litolewa katika katiba mpya. Vilevile amewataka
viongozi wengine kuachana na siasa badala yake kupigania Zanzibar nje ya siasa. Kwani ni siasa ndio
iliyoifikisha hapa Zanzibar.