Aug 3, 2014

MSF: Wakimbizi wa Kiislamu CAR wana hali mbaya

Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limetangaza kuwa, wakimbizi wa Kiislamu katika Jamhuri ya Afrika ya Kati wanakabiliwa na hali mbaya. 

Ripoti ya shirika hilo imebainisha kwamba, maelfu ya wakimbizi wa Kiislamu katika Jamhuri ya Afrika ya Kati wanaishi katika mazingira magumu na mabaya sana baada ya kuyakimbia makazi yao wakihofia usalama wa maisha yao.
Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka limetangaza kuwa, wengi wa Waislamu hao wamelazimika kuyakimbia makazi yao kutokana na kuandamwa na mashambulio ya wanamgambo wa Kikristo wa Anti-Balaka.

 Shirika hilo limeeleza kuwa, zaidi ya watu laki tano wanaishi katika hali mbaya kwenye kambi za wakimbizi zilizoko katika nchi za Chad, Cameroon, Jamhuri ya Kongo Brazzaville na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. 

Inaelezwa kuwa, serikali ya nchi hiyo haina uwezo wa kudhibiti usalama wa Bangui, mji mkuu wa nchi hiyo na hata katika baadhi ya mikoa ya nchi hiyo. Aidha habari kutoka Bangui, mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati zinasema kuwa, hali ya usalama katika mji huo bado haijaboreka licha ya kuweko juhudi za kila upande.

0 comments:

Post a Comment