Aug 17, 2014

Machafuko Marekani baada ya kuuawa kijana mweusi

Machafuko yameendelea Marekani katika mji wa Ferguson, Missouri baada ya vikosi vya usalama kuwashambulia waandamanaji ambao wanalalamikia hatua ya polisi mzungu kumpiga risasi na kumuua kijana mweusi au Mwafrika Mmarekani.
Kijana huyo hakuwa na silaha yoyote wakati wa kupigwa  risasi. 

Ikumbukwe kuwa Agosti  tisa, Michael Brown mwenye umri wa miaka 18 alipigwa risasi  kadhaa na kuuawa na polisi katika mtaa wa St. Louis mjini Ferguson. 

Tokea mauaji hayo ya kibaguzi yajiri kumekuwepo na maandamano kila usiku katika mji huo ambao wakaazi wake wengi ni Wamarekani weusi.

Maandamano dhidi ya ubaguzi wa rangi yameripotiwa  katika miji mingi kote Marekani. 

 Jana Jumaposi kumeripotiwa mapambano mitaani baina ya polisi na wananchi waliokuwa na hasira. 

Polisi wa kuzima ghasia waliokuwa na silaha nzito nzito na magari ya deraya walitumia mkono wa chumba kukabiliana na waandamanaji. 

Maandamano pia yalifanyika Washington DC nje ya Ikulu ya White House ambapo washiriki wamelaani vikali ukatili wa polisi katika kukabiliana na waandamanaji. 

Rais Obama wa Marekani ametoa wito wa utulivu na amewataka polisi waheshimu waandamanaji na wachunguze mauaji ya kijana huyo. 

Pamoja na Marekani kudai ni kinara wa haki za binaadamu lakini vikosi vya usalama nchini humo vinalaumiwa kwa kutekeleza mauaji ya kibaguzi dhidi ya watu wasio na hatia hasa Wamarekani wenye asilia ya Kiafrika.

0 comments:

Post a Comment