Jul 4, 2014

Watu wanne wafariki kutokana na ajali ya ndege Nairobi

Maafisa wa usalama wakagua ndege iliyoanguka mtaa wa Utawala, nairobi Jumatano asubuhi ikielekea Mogadishu
Maafisa wa usalama wakagua ndege iliyoanguka mtaa wa Utawala, nairobi Jumatano asubuhi ikielekea Mogadishu

Watu wanne wameuwawa Jumatano asubuhi baada ya ndege ya mzigo kuanguka katika mtaa wa Utawala mjini Nairobi, na kuharibu majengo mawili kabla ya kuwaka moto.

Walinzi wawili walokua karibu na majengo hayo ya biashara walijeruhiwa, na kutibiwa hospitali. Mkuu wa polisi wa County ya Nairobi Benson Kibue amesema ajali hiyo ilitokea saa kumi alfajiri wakati ndege ya shirika la Skyward kuanguka na kuwaka moto.

Watu wann walokua ndani ya ndege akiwemo rubani ndio waliuliwa, muda mfupi baada ya ndege hiyo kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kenyatta mjini Nairobi ikiwa inasafirisha mizigo wa mirungi kuelekea Mogadishu, Somalia.

0 comments:

Post a Comment