Jul 28, 2014

Kichanga akutwa hai Gaza kwa mama aliyeuawa

Madaktari wa Ukanda wa Ghaza katika hospitali ya Shuhadaaul- Aqsa wamefanikiwa kuokoa maisha ya mtoto mchanga ambaye mimba yake ilikuwa na umri wa miezi nane na nusu kutoka katika tumbo la mama aliyeuawa shahidi kwa hujuma ya ndege za kivita za utawala haramu wa Israel katika ukanda huo.
Kwa mujibu wa kanali ya televisheni ya al-Alam, mtoto huyo aliokolewa baada ya kugundulika kuwa alikuwa angali hai ndani ya tumbo la mama yake, licha ya kwamba mama yake mzazi alikuwa amekwishafariki dunia. 

Habari zaidi zinasema kuwa ndege aina ya F 16 ya utawala haramu wa Israel iliishambulia nyumba aliyokuwa akiishi Shaimaa na Ibrahim (wazazi wa mtoto huyo) na kumuua shahidi Shaimaa huku Bwana Ibrahim akijeruhiwa vibaya katika hujuma hiyo. 

Inaelezwa kuwa baada ya shambulizi hilo, mama wa mtoto huyo aliangukiwa na vifusi vya nyumba iliyokuwa imeharibiwa vibaya. 

Juhudi za waokoaji zilifanikisha kumuondoa mama wa mtoto huyo ambaye wakati huo tayari alikuwa ameuawa shahidi huku mtoto akionekana kuwa hai suala lililowafanya kuuharakisha mwili wa mzazi huyo katika hospitali na kufanikiwa kuokoa maisha ya kichanga hicho.

0 comments:

Post a Comment