Apr 23, 2014

Wazazi waomba Boko Haram kuwa na huruma

Jeshi limekosa kudhibiti kundi la Boko Haram licha ya vita vya mda mrefu dhidi ya kundi hilo
Wazazi na jamaa wa wasichana wa shule waliopotea nchini Nigeria baada ya kutekwa nyara wamewaomba wapiganaji wa kiislamu kuwa na huruma na kuwasihi kuwaachilia watoto wao .

Mkuu wa shule yao anasema zaidi ya wasichana mia moja na nane bado hawajulikana walipo.
Wiki iliyopita wazazi wa wasichana hao waliamka na kupata taarifa kuwa shule ya Chibok ilishambuliwa na wapiganaji wa kiislam na kwamba watoto wao wamepelekwa msituni .
Wachache walibahatika kutoroka , lakini mkuu wa shule hiyo anasema wasichana mia moja na nane bado hawajulikani walipo .

Mmoja wa baba wasichana hao amesema kuwa anatumai serikali itafanya mazungumzo na wapiganaji hao wa kiislamu , kwa sababu anasema anahofu kuwa matumizi ya nguvu itawaweka hatarini zaidi wasichana .

Amewaomba Boko Haram kuonyesha huruma.

La kushangaza ni kwamba maafisa wa Nigeria wamekaa kimya kuhusiana na utekaji nyara huu.

Rais Goodluck Jonathan hajatoa tamko lolote kuhusiana na tukio hili . 

Jeshi linasema linajaribu kuwanusuru wasichana hao , lakini haifahamiki juhudi hizo zimefikia wapi.

0 comments:

Post a Comment