Feb 26, 2014

Obama Kuondoa majeshi yake Afghanistan

Wapiganaji wa Taliban

Rais Obama ameagiza makao makuu ya ulinzi nchini Marekani Pentagon kuandaa mipango ya kuwaondoa wanajeshi wake wote kutoka Afghanistan ifikapo mwisho wa mwaka huu iwapo hakutakuwepo maafikiano rasmi na Serikali ya Afghanistan.

Rais Obama alimpigia simu Rais Karzai wa Afghansitan juu ya mipango hiyo yake.
Rais Karzai amewaudhi Marekani kwa kukataa kata kata kutia sahihi muafaka ambao ungeruhusu baadhi ya wanajeshi kuendelea kukaa Afghanistan baada ya muda uliokubaliwa awali wa mwisho wa mwaka huu wa 2014 .

Mpango huo ambao tayari ulikuwa umekubaliwa na baadhi ya viongozi wa kikabila wa Afghanistan - unaandaa wajibu wa wanajeshi wa NATO unaoshirikisha kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Afghanistan na kusaidia Serikali ya taifa hilo kukabiliana na wapiganaji wa Kitaliban.

Mkataba huo pia unawapa kinga ya kisheria wanajeshi wa Marekani walioko nchini Afghanistan.

Ikulu ya White House inasema kuwa hakuna uwezekano wa Karzai kutia sahihi mapatano hayo kabla ya kuondoka mamlakani Aprili mwaka huu.

0 comments:

Post a Comment