Jan 10, 2014

Wananchi Wachoma Moto Basi La Mtei

 
Basi la abiria la Mtei na pikipiki iliyokuwa imebeba wanafamilia watatu katika mtindo wa mshkaki limeteketea kwa moto na kusababisha kifo cha watu watatu.

Kati ajali hiyo watu wawili walifariki katika eneo la ajali na mwingine kufia njiani wakati anakimbizwa hospitali.

 kwa mujibu wa mashuhuda ni kwamba ajali hiyo iliyotokea saa mbili na nusu Asubuhi katika eneo la minara ya Posta na TBC mkoani Singida, ilisababishwa na dereva wa pikipiki alipokuwa akitaka kukata kona bila kuonyesha ishara ya taa wakati basi la Mtei likiwa linaovateki.
 
Basi la Mtei lililokuwa limebeba abiria wakati limeanza safari ya kuelekea Arusha, ililazimu abiria wote kushuka wao na mali zao wakati wananchi wenye hasira kali walipoamua kujichukulia sharia mkononi kwa kulichoma basi hilo kama linavyoonekana pichani (chini).
 
 
 
 
 
 

0 comments:

Post a Comment