WAFANYABIASHARA 3,980
kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, jana walimuweka kitimoto Waziri wa
Viwanda na Biashara, Dkt. Abdallah Kigoda, wakipinga matumizi ya mashine
za kielektroniki za kutolea risiti (EFD.
Mkutano wa Dkt. Kigoda na
wafanyabiashara hao, ulifanyika Dar es Salaam jana na kudai mchakato wa
kuingizwa kwake nchini haukuwashirikisha kama wadau wa mashine hizo.
Akitoa
msimamo wao , Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wafanyabiashara nchini,
Bw. Philimin Chonde ilisema hawakatai kulipa kodi bali wanapingana na
Serikali kuhusu matumizi ya mashine hizo kwani hazipo katika mfumo
mzuri.
Alisema mashine hizo zinaonesha zaidi mauzo kuliko faida na
hasara ambazo wanazipata hivyo hizo ni kasoro zilizopo katika mfumo wa
matumizi yake, ukosefu wa mtandao na haitunzi umeme wa kutosha.
"Tunakuomba
Mheshimiwa Waziri,utufikishie salamu zetu kwa Rais Jakaya Kikwete,
tunataka aunde tume huru ambayo itashirikisha wafanyabiashara, wachumi,
ofisi ya Rais na washauri wa masuala ya biashara.
"Tume hii ifanye
kazi miezi sita ili kubaini kasoro ambazo zimejitokeza katika mchakato
mzima wa utumiaji mashine hizo ili tufikie mwafaka," alisema.
Bw.
Chonde pia alimtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu,
kuhakikisha baadhi ya askari ambao hufanya doria kwa pikipiki mitaani
wanaacha tabia ya kuwatisha wafanyabiashara, kuomba na kupokea rushwa
hasa baada ya kuingia mashine hizo.
"Mashine hizi zimeleta ulaji kwa
askari polisi, wanashirikiana na Maofisa TRA kutukamata na kututoza
kodi kinguvu sawa na mradi wa kufunga vidhibiti mwendo kwenye mabasi,"
alisema.
Waliitaka Serikali ikaenao pamoja ili wapeane mbinu za
kuongeza ukusanyaji kodi pasipo kutumia mashine hizo ambazo zimekuwa
mradi wa watu fulani jambo ambalo linawezekana.
Akijibu hoja hizo,
Dkt. Kigoda alisema amepokea hoja hizo na atazifikisha kwa Rais kwani
yeye ni sehemu ya wafanyabiashara hao na mambo yaliyosemwa ni ya msingi
kwa mustakabali wa Taifa.
"Ndugu zangu, kazi yangu ni kuisukuma
Serikali iweze kupunguza gharama za biashara kiuchumi hivyo nimechukua
maoni yenu nitamfikishia Rais.
"Matatizo ya uchumi yanamalizwa kiuchumi si kidini wala kisiasa hivyo naahidi kuyafanyia kazi matatizo yote," alisema.
Mvutano
kati ya Serikali na wafanyabiashara nchini, ulianza baada ya Mamlaka ya
Mapato (TRA), kuweka utaratibu mpya wa ukusanyaji wa kodi kwa kutumia
mashine za EFD
0 comments:
Post a Comment