Jan 6, 2014

Taarifa ya Serekali Kuhusi Ajali ya Boti ya Kilimanjaro 2



Watu 10 wafariki dunia ajali ya boti Tanzania
TAARIFAA YA SERIKALI KUHUSU TUKIO LA AJALI YA KUDONDOKA ABIRIA WALIOKUA WAKISAFIRI KUTOKA PEMBA KUJA UNGUJA LEO TAREHE   05-01-2014 KWA BOTI YA KILIMANJARO II

Ndugu Wanahabari

Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, tumewaita muda huu kuwaeleza kwa majonzi makubwa kuhusu tokeo la ajali ya kudondoka kwa baadhi ya abiria waliokua wakisafiri kutoka Pemba kuja Unguja, kwa boti ya MV.  Kilimanjaro II.


Ndugu Wanahabari

Kunako majira ya saa 3:00 za asubuhi wakati boti hiyo ikiwa safarini kutoka Pemba kuja Unguja ilipofika katika   maeneo ya bahari ya Nungwi ilikumbwa na mawimbi makali, mawimbi ambayo yalisababisha baadhi ya abiria waliokuwa wamekaa nje sehemu ya mbele kusombwa na mawimbi na kudondoka baharini.


Ndugu Wanahabari

Baada ya kutokea tukio hilo, vyombo vya Serikali vikisaidiwa na wananchi wa Nungwi na wa maeneo ya jirani walifika katika eneo la tukio kwa ajili ya kufanya uokozi. Katika zoezi hilo, vyombo hivyo vimefanikiwa kuokoa watu watatu (3) wote wanaume watu wazima wakiwa wako hai na hali zao zinaendelea vizuri katika hospitali ya Mnazi Mmoja. Aidha, jumla ya maiti watano (5) wamepatikana. Kati ya hao, wanaume watatu (mmoja mtu wazima na wawili watoto) na wanawake wawili (mmoja mtu mzima na mmoja mtoto).

0 comments:

Post a Comment