TAARIFAA YA SERIKALI KUHUSU
TUKIO LA AJALI YA KUDONDOKA ABIRIA WALIOKUA WAKISAFIRI KUTOKA PEMBA KUJA UNGUJA
LEO TAREHE 05-01-2014 KWA BOTI YA
KILIMANJARO II
Ndugu Wanahabari
Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa
Rais, tumewaita muda huu kuwaeleza kwa majonzi makubwa kuhusu tokeo la ajali ya
kudondoka kwa baadhi ya abiria waliokua wakisafiri kutoka Pemba kuja Unguja,
kwa boti ya MV. Kilimanjaro II.
Ndugu Wanahabari
Kunako majira ya saa 3:00 za asubuhi wakati boti hiyo ikiwa
safarini kutoka Pemba kuja Unguja ilipofika katika maeneo ya bahari ya Nungwi ilikumbwa na
mawimbi makali, mawimbi ambayo yalisababisha baadhi ya abiria waliokuwa wamekaa
nje sehemu ya mbele kusombwa na mawimbi na kudondoka baharini.
Ndugu Wanahabari
Baada ya kutokea tukio hilo, vyombo vya Serikali vikisaidiwa
na wananchi wa Nungwi na wa maeneo ya jirani walifika katika eneo la tukio kwa
ajili ya kufanya uokozi. Katika zoezi hilo, vyombo hivyo vimefanikiwa kuokoa
watu watatu (3) wote wanaume watu wazima wakiwa wako hai na hali zao
zinaendelea vizuri katika hospitali ya Mnazi Mmoja. Aidha, jumla ya maiti
watano (5) wamepatikana. Kati ya hao, wanaume watatu (mmoja mtu wazima na
wawili watoto) na wanawake wawili (mmoja mtu mzima na mmoja mtoto).
0 comments:
Post a Comment