Jan 5, 2014

NYUMBA ZATEKETEA PEMBA,MISAADA YAHITAJIKA








Moja kati ya nyumba 14 katika Kijiji cha Shumba Mjini Wilaya ya Micheweni ziliztoathirika kwa moto mkubwa ulitokea majira ya saa 5.00 asubuhi ya jumapili huku wakaazi wake wakichanganyikiwa kutokana na maafa hayo. Baadhi ya wananchi 100 ambao nyumba zao 14 zimeathirika na vibaya na moto katika Kijiji cha Shumba Mjini wakipata hifadhi kwenye madrasa moja Kijijini hapo.

Moja kati ya nyumba 14 zilizoathirika na moto katika kijiji cha Shumba Mjini ambapo wakaazi wake wakiwa wamechanganyikiwa kutokana na janga hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Shehani Mohd Shehani akitoa tathmini ya awali ya uchunguzi wa moto uliotokea Shumba Mjini mbele ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Sei aliyefika kijijini hapo kuwapa pole wananchi walioathirika na maafa hayo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameiagiza Serikali ya Mkoa wa Kaskazini Pemba kufanya tathmini mara moja nyumba zote zilizoathirika kutokana na moto mkubwa uliokikumba Kijiji cha Shumba Mjini leo majira ya saa 5.00 za asubuhi.
 
Nyumba zipatazo 14 zikiwa na wakaazi 100 zimeathirika vibaya kutokana na moto huo na nyengine  24 kuezuliwa mapaa yake kwa hofu ya kuathirika na moto huo ambao hadi sasa kwa mujibu wa taarifa za Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Shehani  Mohd Shehani kwamba chanzo chake bado hakijafahamika huku uchunguzi wa jeshi la polisi pamoja na vikosi vyengine vya ulnzi ukiendelea.
 
Balozi Seif ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Maafa Zanzibar akiwa kisiwani Pemba kwa shughuli mbali mbali za Maadhimisho ya Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar alitoa agizo hilo muda mfupi baada ya kuwafariji  wananchi wa Kijiji cha Shumba Mjini kutokana na maafa waliyoyapata ya janga la moto.
 
Akiwapa pole wananchi hao 100 waliohifadhiwa kwenye madrasa mmoja Kijijini humo na baadaye kupelekwa Skuli ya Kijiji hicho Balozi Seif aliwataka kuwa na subra katika kipindi hichi cha mitihani na Serikali inajipanga kuangalia namna ya kuwasaidia wananchi hao.
 
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaandaa kikao maalum cha dharura keshokutwa jumatatu ili kulijadili suala hili na kuona jinsi itakavyoweza kukusanya nguvu za kuwasaidia wananchi walioathirika na janga hili.
 
MUNIRA BLOG INAWAPA POLE.

0 comments:

Post a Comment