MATUKIO ya utekaji
watu, kuwatesa na kuwatelekeza,yameanza tena baada ya Mwenyekiti wa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilaya ya Temeke, Dar es
Salaam, Bw. Joseph Yona, kutekwa, kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili
na kutupwa eneo la Ununio, Tegeta, Dar es Salaam.
Tukio hilo lilitokea saa 5 usiku wa kumakia jana baada ya watekaji hao, kumkuta Bw. Yona eneo Mtoni kwa Azizi Ally, Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam.
Bw. Yona alikuwa amekaa katika tawi la chama hicho na watu wengine sita wakiwa katika mazungumzo ya kawaida.
Akizungumza na
waandishi wa habari katika Kitengo cha Taasisi ya Mifupa (MOI),
kilichopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), ambako amelazwa,
Bw. Yona alisema sababu ya kutekwa kwake na kutezwa ni baada ya kuitisha
mkutano na wahandishi wa habari.
"Mkutano huu niliuhitisha katika Hoteli ya Lamada, Ilala,Dar es Salaam uliokuwa ukijadili sakata la kuvuliwa uongozi Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe katika chama ndipo nilipoanza kutishwa kila wakati.
"Uongozi wa chama Makao Makuu ulitaka kuning'oa katika nafasi yangu lakini Kamati ya Utendaji ilikataa na kudai hawaoni kosa langu ni lipi...lilitoka agizo kwa viongozi wakuu wa chama kutaka ofisi yangu Temeke ifungwe," alisema.
Aliongeza kuwa, siku ya tukio saa 5 usiku akiwa eneo la Mtoni kwa Azizi Ally akizungumza na watu watatu, aliona kundi la watu sita likifika eneo hilo na kusema wanataka kumkamata yeye si watu wengine aliokuwa amekaa nao.
Bw. Yona alisema, alipowauliza wametumwa na nani kumkamata walidai ni maagizo ya viongozi wakuu wa CHADEMA, kutokana na mkakati wake wa kumuunga mkono Bw. Kabwe ambaye alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho.
"Walinikamata na kudai wananipeleka Kituo cha Polisi Kati kwenda kutoa maelezo zaidi lakini nilishangaa kuona gari likipita kituoni na kwenda eneo ambalo sikulijua.
"Tulipofika eneo ambalo sikulifahamu, nilivuliwa fulana na kuzibwa machoni, walianza kunipiga na kunihoji wakinitaka niachane na shughuli za chama ili wasiniue," alisema.
Aliongeza kuwa, hakuweza kuwajibu kitu bali aliwaambia kuwa, kama wanataka maelezo zaidi kuhusu Kabwe waende wakamuulize mwenyewe kwani yeye hawezi kumsemea.
"Nilipojibu hivyo, mmoka kati ya watekaji alinipiga na kitu chenye ncha kali kichwani akiwa amenibinya sehemu zangu za siri...nilisikia maumivu makali nikawambia kwa nini mnaniua na mimi nina familia kama nyinyi.
"Muda huo tayari nilikuwa nimepigwa na kitu kizito, kupoteza fahamu hivyo walikimbia wakijua nimepoteza maisha, nilikuja kuamka saa 10 alfajiri na kujikuta niko peke yangu, nguo zangu zilikuwa zimetapakaa damu," alisema Bw. Yona.
Alisema baada ya kujitambua, alikwenda kugonga hodi katika nyumba ziliyopo jirani na eneo hilo ili kuomba msaada.
"Nilijitahidi kugonga milango milangu katika nyumba tatu lakini sikufunguliwa hivyo niliamua kujisogeza kidogokidogo ili nisubiri kukuche niombe msaada kwa watu wengine.
"Ilipofika saa 11
alfajiri, katia nyumba nilizogonga mlango kuna mtu alitoka, kunifuata na
kuniuliza shida yangu ndipo nikamwambia...anilitaka nitaje namba ya mtu
wangu wa karibu nikampa ya mdogo wake anaitwa Ayubu," alisema.
MOI wazungumza
Msemaji
wa MOI, Bw. Patrick Mvungi, alisema walimpokea Bw. Yona saa 5 asubuhi
akitokea MNH akiwa tayari amefanyiwa kipimo cha TC-SCAN hivyo bado
anaendelea na matibabu.
Polisi watoa tamkoKutokana na tukio la kutekwa Bw. Yona, ambaye ni kitaaluma ni Mtaalamu wa Maabara Chuo Kikuu cha Elimu (DUCE), Dar es Salaam, kupigwa na kujeruhiwa, Jeshi la Polisi Kanda







0 comments:
Post a Comment