Umoja wa Masheikh na Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania kupitia Katibu Mkuu wake, Hamis Mataka amelitaka Jeshi la
Polisi Zanzibar kuwajibika ipasavyo na kuwapata watu waliohusika na
unyama huo dhidi ya Padre wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Zanzibar, Anselmo Mwang’amba
Sheikh Mataka alisema kama
matendo ya kinyama ya watu kumwagiwa tindikali hayatafanyiwa kazi na
mzizi wa uasi huo kuchimbuliwa amani ya nchi itatoweka.
“Lazima Jeshi la Polisi lifanye kazi yake kwani hali si nzuri na
kutokana na matukio hayo kufululiza. Kimsingi matukio haya yanaweza
kuzua hisia mbaya za udini na uzanzibar na ubara, hivyo yakomeshwe mara
moja,” alisema Sheikh Mataka.
Alisema vyombo vya dola vinapaswa kutimiza majukumu yake ya kulinda
amani na mali za watu vinginevyo historia ya Zanzibar kwamba ni eneo
tulivu lenye amani itatoweka na kuonekana kuwa ni eneo lisilofaa kuishi
kwa watu ambao si wazawa wa eneo hilo.
Shekh Mataka alitumia nafasi hiyo kutoa pole kwa Padre Mwang’amba na
kwamba yeye kama kiongozi wa dini hataacha kuonya na kuelekeza kisha
kuwaachia wahusika kutenda sawasawa na nafasi zao zinavyowataka
kuwajibika.
RAIS WA SERILKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR MHE DK MUHAMMED SHEIN AKIMJULIA HALI PADRI MWANG'AMBA.
RAIS WA SERILKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR MHE DK MUHAMMED SHEIN AKIMJULIA HALI PADRI MWANG'AMBA.
0 comments:
Post a Comment