SAKATA
LA SHEIKH PONDA
·
WAIKATAA TUME YA
POLISI,WATAKA TUME HURU,
·
KAMANDA SHILOGILE
NA WENZAKE WASHITAKIWE
·
WAZIRI NCHIMBI
ATAKIWA KUJIUZULU.
Na
mwandishi wetu wa munira;
Hatimaye Waislamu
nchini Tanzania
wametoa Tamko kufuatia tukio la kikatiri la kupigwa risasi Sheikh Ponda Issa Ponda
mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki
iliyopita.
Hayo yamesemwa
jioni hii na Sheikh Kondo Juma Bungo alipokuwa akizungumza na maelfu ya Waislamu
waliofurika katika viwanja vya Mwembe Yanga vilivyopo Tandika Jijini Dar
salaam.
Amesema Sheikh “Ponda Issa Pondo hakupigwa risasi kwa bahati
mbaya,Serikali inayoongozwa na CCM ilidhamiria kumpiga risasi Sheikh Ponda na
lengo lao lilikuwa ni kumuuwa lakini kwa Rehma za ALLAAH Sheikh Ponda
amenusurika labda wammalizie huko alipo”mwisho wa kumnukuu.
“Ndugu Waislamu kwa nini nasema walikusudia,taratibu
za kumkamata kiongozi awe wa dini au wa kisiasa zipo wazi,mbali ya hayo
nyumbani kwake wanapajuwa,lakini kwa kuonesha kwamba walikusudia,vituko vyao vilianza
siku ya Iddi mosi mimi na Sheikh Ponda tulikuwa ni miongoni mwa tulioshiriki
katika Baraza la Idd pale Kichangani,tukiwa ndani ya Baraza la Idd,tukapigiwa
simu kutoka Jeshi la polisi kwamba marufuku Sheikh Ponda kuongea,tukajiuliza
kwa nini asiongee,sisi tukasema lazima aongee na aliongea”alisema
Sheikh Kondo
aliendelea kuuzindua umma kwa kusema “mara
baada ya Baraza la Idd kumalizika,jioni ile ile tukaenda Morogoro mimi,Sheikh Ponda
na dereva wetu.Viongozi wa Waislamu wa Mkoa wa Morogoro wakaomba kibali Jeshi
la Polisi na wakaruhusiwa,tukiwa ndani ya Mhadhara tukaletewa taarifa kutoka
Polisi kwamba Sheikh Ponda asiongee,mara tukaona vikosi vya Usalama vinazidi
kuongezeka,tulipo maliza na kuanza kuondoka magari ya polisi yakaanza kutufuata,nikakubaliana
mimi na Sheikh Ponda ambao tulikuwa viti vya nyuma ya kwamba hawa wamekusudia shari,sasa
kila mtu aangalie namna ya kufanya.Nikiwa umbali wa mita mia moja nikapata
taarifa ya kwamba Ponda kapigwa risasi”
“Ndugu zangu tukiangalia Historia ya huko
tulipotoka inaonyesha kwamba hii Serikali ya CCM kupitia Jeshi la Polisi wanatabia
ya kuua hovyo hasa kwa waislamu,sasa wamekusudia kutumaliza sisi waislamu
wakiamini kwamba hiyo ndiyo njia ya kutuzuwia tusiyaweke wazi madai yetu,lakini
napenda wafahamu kwamba japo Sheikh Ponda hajafa lakini damu yake ni lazima
ilipwe,na hata wakimuua Sheikh Ponda lakini hatutorudi nyuma na tutazidi
kufichua dhulma tunazofanyiwa waislamu”.
Akitoa msimamo wa
Wasilamu Sheikh Kondo alisema “Tunaitaka Serikali ifanye mambo matatu,Iunde
tume huru itakayochunguza kadhia hii kwa uadilifu na uwazi (hatuitaki wala
kuitambua tume iliyoundwa na Jeshi la polisi).
Kamanda wa polisi
wa Mkoa wa Morogoro Faustine Shilogile afikishwe mahakamani yeye na kiongozi wa
Opresheni katika tukio hilo.
Waziri wa ulinzi Mhe Nchimbi naye ajiuzulu.
HILI NDILO JERAHA LA RISASI KATIKA MWILI WA SHEIKH PONDA.
TAKBIIR,WAISLAMU WAKISIKILIZA TAMKO WAKATI SHEIKH KONDO AKIWASILISHA TAMKO HILO JIONI HII.