- AITAKA SERIKALI IUNDE TUME HURU.
- IKIWA NI KWELI,POLISI IMEJENGA MAHUSIANO MABAYA NA WAISLAMU;AL HAD.
- YASEMWA DAMU YAKE KUWA UKOMBOZI KWA WAPIGANIA HAKI ZA WAISLAMU.
- WAPIGANIA HAKI HUU SIO UGAIDI?
Na mwandishi wetu wa
munira.
Serikali imetakiwa
kumkamata polisi aliyempiga risasi katibu wa Baraza Kuu la Taasisi na Jumiya za Kiislamu
nchini Sheikh Ponda Issa Ponda ikiwa inazingatia haki na utawala bora.
Hayo yamesemwa na
mwenyekiti wa Baraza kuu la Taasisi na Jumuiya za Kiislamu nchini ambaye pia ni Amir wa Shura ya Maimamu Shekh Yusuf Kundecha alipokuwa akizungumza na waandishi
wa habari katika msikiti wa mtambani.
Amesema tukio la kumpiga
risasi Sheikh Ponda ni tukio la kikatiri linalopingana na sheria za haki ya kibinaadamu
na haliendi sawa na dhana ya Demokrasia na utawala bora.
"Sisi tunasema tunaitaka
serikali hii ikiwa ina sifa ya usikivu basi imkamaete na imfikishe katika
vyombo vya sheria askari polisi aliyempiga risasi sheikh ponda bila ya hivyo
hatutoilewa serikali".
Aidha alivishukia baadhi ya vyombo vya habari kwa kupotosha habari na kusema hawatendi haki kwani wana wanyima wananchi habari za kweli lakini baya zaidi wanaweza kuiingiza nchi katika matatizo.
Aidha alivishukia baadhi ya vyombo vya habari kwa kupotosha habari na kusema hawatendi haki kwani wana wanyima wananchi habari za kweli lakini baya zaidi wanaweza kuiingiza nchi katika matatizo.
Kwa upande wake Sheikh
Juma Ramadhan ambaye alikuwa ni mmoja miongoni mwa masheikh waliozungumza na Waislamu waliojazana katika msikiti huo alisema ,"Mtume S.A.W. amesema vitu
vitatu viheshimiwe mali za waislamu zisichezewe,heshima ya waislamu isichezewe na damu ya
muislamu isimwagwe hovyo,leo katika nchi hii imejengeka tabia ya kumwaga mwaga
damu za waislamu,tuna sema damu hii ya Sheikh Ponda ndiyo itakuwa ukombozi
katika kupigania haki za waislamu katika nchi hii".
Akiongea na waandishi
wa habari ofisini kwake Sheikh wa mkoa wa Dar es salaam Al Had Mussa Salum
amesema "ikiwa ni kweli polisi wamempiga risasi Sheikh Ponda,basi itakuwa imefungua mahusiano
mabaya na waislamu" na kuongeza kwa kusema wao kama Bakwata haina uadui na Sheikh Ponda japo wana tofautiana katika mawazo.
Kwa upande mwengine
waislamu mbalimbali wamejitokeza kutoa maoni yao baada ya kuguswa na tukio la kupigwa risasi Sheikh Ponda ,”alipouwawa Padri
kule Zanzibar waziri wa ulinzi na wapigania haki mbalimbal walisema huu ni
ugaidi na wakaitwa FBI waje kuchunguza,yalipochomwa moto makanisa wakasema tena
kwamba huu ni ugaidi,lilipolipuka bomu kanisani wakasema tena kwamba huu ni
ugaidi,lakini hili la kupigwa risasi Sheikh Ponda wote hao wamefunga midomo yao
juu ya neno ugaidi,tunakwenda wapi,ina maanisha nini”alisema muumini mmoja
kwa uchungu mkubwa.


HAWA NI SEHEMU YA WAISLAMU WALIOJAZANA NDANI NA NJE YA MSIKITI WA MTAMBANI KUSIKILIZA TAMKO LA VIONGOZI WA WAISLAMU BAADA YA SHEIKH PONDA ISSA PONDA KUPIGWA RISASI